Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, November 9, 2012

Afungwa miaka 40 Afrika Kusini kwa pembe za vifaru

Picha mbali mbali za mizoga ya faru ambao ambao wameuwawa 
kwa sumu na kuondolewa pembe

By Goldentz.blogspot.com
Friday, Nov. 09, 2012.

Vifaru wanakabiliwa na tisho la kuwindwa kiharamu
Mahakama nchini Afrika Kusini imemhukumu kifungo cha miaka arobaini raia mmoja wa Thailand aliyepatikana na hatia ya kuuza pembe za vifaru na kuandaa maonyesho ya uwindaji yasiyokubalika
Chumlong Lemtongthai alikiri kosa la kuwalipa makahaba kuweza kufanya maonyesho ya uwindaji wa vifaru.
Pembe hizo ziliuzwa barani Asia ambako soko la pembe hizi ni kubwa sana kwani hutumiwa kama dawa.
Zaidi ya vifaru miatano wameuawa nchini humo na wawindaji haramu mwaka huu pekee.
Akitoa hukumu hiyo jaji alisema kuwa hataki wajukuu wake wakuwe bila kujionea vifaru nchii humo.
Tanzania bado tunapiga bla bla tu kwenye hili. Tunatakiwa kuiga mfano wa Afrika Kusini katika kukabiliana na uharamia katika mbuga zetu. Tunasikia tu watu wanakamatwa lakini hawatajwi kwa majina hata kusikia wamepewa hukumu kali kama fundisho. Tuige mfano wa Afriak Kusini kuwaonyesha hadharani ili wajukuu wetu wajue kuwa Tanzania haina faru tena kutokana na uharamia wa fulani bin fulani. 
 

  

 


 

Kitoto cha faru kikiwa hakijui la kufanya baada ya mama yake 
kuuwawa na maharamia kwa ajili ya pembe

 

 
Bango likimwonyesha  haramia Chumlong Lemtongthai raiya 
wa Thailand aliyehukumiwa miaka 40 kwa kuua faru.

 

 
Haramia Chumlong Lemtongthai akiwa mahakamani Afrika Kusini

 

 
baadhi ya pembe za faru zilizokamatwa

  
Haramia  Chumlong Lemtongthai akiwa mahakamani na mawakili wake



  

  
 Haramia Chumlong Lemtongthai 


Source: GoldenTzblog

No comments :

Post a Comment