DR.SLAA TAMBUA MWOSHA HUOSHWA
UMEWADANGANYA watanzania vya kutosha, umewapandikiza chuki na kuwafitinisha vya kutosha, haujaweza kuwashauri kufanya kazi zaidi ya maandamano, umewaburuza vya kutosha ndani ya chama na umewagawa vya kutosha sasa wamejitambua waachie chama chao waendelee. Kwa wafuatiliaji wa siasa za hapa Tanzania wengi hata huku kwetu Nyikani, tunajua kuwa katibu wa Chadema Taifa Dr, Wilbroad Slaa amewapa vyeo kwa upendeleo waliokuwa ‘’wanamlamba’’ miguu yeye pamoja na mchumba wake Josephine Mshumbushi. Padri Dr, Slaa mbali na hayo amevunja katiba ya Chadem vya kutosha, amevuruga chaguzi za ndani ya Chadema vya kutosha, wanachama wengine wameondoka kundini ikiwa ni pamoja na kushindwa kuendelea kukisaidia chama hicho kwasababu yake na wengine wamekonda miili na akili, wengine wameumizwa na vyombo vya dola kutokana ushawishi wa kutotii sheria bila shuruti. Tunakumbuka pale mkoani Mbeya mtu huyu huyu yaani Padre Dr. Slaa aliposababisha mnyukano mkali mpaka leo kwa viongozi wa Chadema baada tu ya kumalizika ziara yake Januari 13,2012 baada ya Dr. Slaa kuwapora demokrasia wanaChadema mkoa wa Mbeya kwa kumvua madaraka aliyekuwa katibu wa chama hicho mkoani humo Mwanasheria Eddo Mwamalala na kumpachika cheo cha ushauri wa mkoa.
Kwa akili zake alifanya makusudi kwa kujua wazi kuwa hakuna wa kuhoji maana anatumia mbinu ile ile ya kuwagawa kisha kuwatawala vizuri huku baadhi akiwaahidi neema kwenye chama hicho. Baada ya kumuondoa Mwamalala katika nafasi ya ukatibu wa mkoa, akampachika Boid Mwabulanga kushika nafasi hiyo ambayo masikini mtu huyo hajawahi kuiota wala kuiomba kwa mujibu wa katiba ya Chadema kisha akapigiwa simu kuwa anaikubali au anaikataa nafasi hiyo jambo ambalo lilimshitua sana Mwabulambo ambaye hawezi kushawishi vijana kuandamana pasipo kuangalia maslahi ya wananchi kwanza. Kutokana na hali hiyo Mwabulanga anaendelea kuishikilia nafasi hiyo kwa ushahidi tu maana haivi chungu kimoja na baadhi ya viongozi wenzake ambao wamejazwa fikra za kuendesha chama hicho chenye mvuto kwa walio kata tamaa kwa mtindo wa sinema za vurugu. Hakuishia hapo, kwa kujua kuwa Mbeya hakuna anayekijua vema chama hicho na chama hicho sawa na mali ya watu fulani alifanya mamuzi ya kumpachika cheo cha Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Mbeya Peter Mwamboneke kana kwamba anataka kumvalisha viatu vikubwa alivyoviacha mwanasheria Sambwee Shitambala ambavyo mpaka sasa nafasi hiyo hakuna aliyeweza kuimudu. Wanachama ambao walijitokeza kuwania nafasi hiyo ni pamoja na John Mwambigija ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Mbeya Mjini na rafiki mkubwa wa familia ya Dr.Slaa, Zabron Nzunda (Sabodo), Mwanasheria Philipo Mwakilima(Crimax) na Mwanasheria John Ngeka. Wengine walikuwa ni Joseph Mwachembe(China), George Mtasha, Herode Jivava, Hugho Kimario, Aminika Mwihomeke na mwanadada pekee Sorwa Gea. Katika uchaguzi huo rafiki wa Dr, Slaa na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi, John Mwambigija, alionekana kuzidiwa na dalili zilionesha kuwa asingeweza kushinda bali nyota ilikuwa ikiwaka kwa Zabron Nzunda aliyekuwa akiungwa mkono na Eddo Mwamalala. Uchaguzi huo ulikuwa ukitarajia kufanyika Juni 20 mwaka huu lakini ukavurugwa na kuvurugika mpaka leo hapo ndipo inajidhihilisha kuwa uzuri wa paka si rangi yake bali ujuzi wa kukamata Panya. Katika kikao kilichoketi Januari 11, mwaka huu katika ukumbi wa hotel ya Mount Livingstone Jijini Mbeya chini ya Dr, Slaa, mfuasi wake w karibu kwa mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chedema wilaya ya Mbeya Mjini John Mwambigija alimtuhumu Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Chunya George Mtasha kuwa ni mla rushwa na hiyo yote inaelezwa kuwa alipata nguvu kutoka kwa ‘’Stering’’ wao. Baada ya mbegu hiyo ya kutaka kuwatimua wote ambao wanaonekana kuwa kikwazo kwa kundi la Dr. Slaa, kilifanyika Kikao cha kumvua uongozi Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Chunya Februari 10, mwaka huu wilayani Chunya na kuongozwa na Mwenyekiti masalia wa chama hicho Peter Mwamboneke. Baada ya kugonga mwamba wilayani Chunya, ukapangwa mkakati mwingine mfu wa kwenda kumuondoa Mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya Mbeya Vijijini Eliah Kabholile kutokana na maelewano hasi na Dr. Slaa lakini pia mkakati huo ukashindikana baada ya mtandao huu wa www.kalulunga.blogspot.com kufichua siri hiyo. Siwezi kunyamaza bila kusema haya kwa ulimwengu maana najua mahala pa kumshitaki Dr. Slaa hata ndani ya chama hakuna maana wengi amewaweka na kulazimisha wawe wanalipwa mishahara hivyo hawawezi kumfanya lolote wala kumhoji lakini kwa nguvu ya kalamu na wanyonge asiowapenda ndani ya Chadema anapaswa kusema yatosha. Tena ana bahati kubwa Zitto Kabwe ni mvumilivu laiti kama angeamua naye kuweka mkono wake kwa wanachadema wanaomkataa Dr, Slaa hakika angekonda sana, lakini amshukuru Mungu kwa hilo. Dr. Slaa amemtumia mchumba wake mara kadhaa kwenda mikoani huku akipokelewa kama kiongozi wa Chadema Taifa wakati hatujui hata nafasi yake ndani ya chama, bila aibu anapokelewa na wafuasi wake kwa kutumia pesa na magari ya kuomba kwa wanachama kana kwamba chama kinamtuma!. Kuna wanachama masalia wa Chadema ambao wanaona Dr, Slaa kusemwa kwa uovu wake na viongozi wenzake ni kama dhambi na inawauma kwelikweli!! Jibu lake ni kwamba hakuna kitu kibaya kama dhambi ya uongo na fitina kwa mtu mzima na mara kadhaa Mungu anaamua kuuangusha ‘’uongozi’’ hasi. Dr, Slaa analijua hili kwa kina, na kabla sijamalizia tayari yeye amekumbuka kuwa kabla hajamkana Mungu alisoma vema kuwa chanzo cha wajenzi wa Mnara wa Babeli kutofautiana lugha kilikuwa ni dhambi na mawazo hasi. Nasema Dr, Slaa mwosha huoshwa kwasababu wale ambao aliwatendea kwa hila wameamua kumlipa kwa hila baada ya kujitambua na nimkumbushe Dr, Slaa kuwa katika Biblia tunaambiwa kuwa Elisha akamwambia Geazi kuwa walio nyuma yetu ni wengi kuliko unaowaona hivyo umefika wakati wa kupima hoja zao badala ya kutegemea wanachama masalia ambao wanamshinikiza kubaki katika nafasi hiyo ili aendelee kulinda maslahi yao.
Mwandishi wa makala haya anapatikana kwa simu 0754 440749 kalulunga2006@yahoo.com
Chanzo: Mwanabidii Forum
Chanzo: Mwanabidii Forum
No comments :
Post a Comment