Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, January 18, 2013

CCM: Nchemba ahofia ajira za wabunge CHADEMA

 Naibu Katibu Mkuu CCM Ndugu Mwigulu Nchemba akikaribishwa katika makao makuu ya CCM Kibaha na Mbunge wa Kibaha Mjini Nd. Silvestry Koka.
17 Jan 2013

Na Benedict Kaguo

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Bara, Bw. Mwigulu Nchemba, amefichua siri ya kutoyaweka bayana majina ya wabunge saba
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), walioomba kujiunga na chama chao.

Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana, Bw. Nchemba alisema hali hiyo inatokana na ukweli kwamba, kama majina hayo yatawekwa hadharani, wabunge hao wanaweza kufukuzwa uanachama ila wakati ukifika watatajwa.

Bw. Nchimba aliyasema hayo kutoa ufafanuzi wa taarifa alizotoa hivi karibuni kuwa wabunge saba wa CHADEMA waliiomba kujiunga na CCM ambapo hali hiyo iliacha maswali mengi
kwa wananchi kutaka kuwafahamu wabunge hao.

“Idadi hii ya wabunge bila kutia shaka wako saba...miongoni mwao watano wanatoka kwenye majimbo, wawili Viti Maalumu ambao wameomba wasitajwe majina wakihofia kupoteza nafasi walizonazo kwa sasa,” alisema Bw. Nchemba.

Aliongeza kuwa, mbunge mmoja wapo wa majimbo anatokea mikoa ya Kanda ya Kaskazini ambapo sababu kubwa ya kutaka kuhamia CCM ni kutokana na mgogoro ulioko ndani ya CHADEMA na kusababisha baadhi ya wanachama kufukuzwa.

“Muda ukifika majina ya wabunge hawa nitayaweka hadharani na sisi tutawapa nafasi ya kugombea majimbo hayo kwa tiketi ya CCM, chama chetu kitaendelea kuwa kinara wa demokrasia nchini kwa kukubadili kubadilika ili kuendana na matakwa ya wananchi,” alisema.

No comments :

Post a Comment