TAARIFA YA MSIBA
Blogu la 'Zanzibar Ni Kwetu' linakupeni pole sana Ndugu Yan Sow na Diddy Sow
na wote waliohusika na msiba huu kwa kupoteza mama yenu mpenzi!
Mungu amlaze pema peponi - Amen!
Familia ya ndugu Demba Sow, inasikitika kutangaza Kifo cha mke wake mpenzi Monique Demba Sow Kasongo. Kilichotokea Burhani Hospital 14-1-13 saa 2 usiku.
Habari ziwafikie watoto wa Marehemu, Yan Sow na Didy Sow walipo America na Canada, ndugu, jamaa na marafiki popote walipo.
Nyumbani kwa Marehemu ni Mikocheni karibu na Clouds Fm.
Mazishi ni kesho Jumamosi 19-1-13 ambapo Misa ya kumuombea Marehemu itafanyika nyumbani kwake Mikocheni tarehe 19-1-13 saa 5 na kuagwa.
Mwili utazikwa Katika makaburi ya Kinondoni saa 9 mchana.
Kwa mawasiliano zaidi,Wasiliana na mwenye namba hii 0754280895
Mungu aiweke Roho ya Marehemu Mahala pema Peponi.
-Amen.
Chanzo: Vijimambo
No comments :
Post a Comment