dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, January 22, 2013

ZANZIBAR: Umeme wakatisha shughuli za baraza

Jengo la Baraza la Wawakilishi ambalo limegharibu fedha nyingi katika ujenzi wake
Jengo la Baraza la Wawakilishi ambalo limegharibu fedha nyingi 
katika ujenzi wake
Na Salma Said
KIKAO cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea Chukwani Mjini Unguja kimelazimika kusitishwa kwa muda kutokana na hitilafu ya umeme iliyotokea katika ukumbi wa baraza hilo la wawakilishi hapo jana asubuhi.
Akitoa tangazo kwa wajumbe wa baraza hilo Spika wa Baraza hilo, Pandu Ameir Kificho aliwaambia wajumbe kwamba kutokana na khitilafu hiyo kikao hicho anakiakhirisha hadi jioni ili kutoa fursa kwa mafundi wa umeme kuja kufanya matengenezo katika ukumbi huo.
Spika Kificho alisema licha ya kuwachwa jenereta na kuendelea na shughuli za baraza hilo lakini kutokana na ukumbwa na mahitaji makubwa ya umeme katika ukumbi huo majenereta hayo hayana uwezo wa kumaliza shughuli zima ya vikao vya baraza hilo na hivyo wanalazimika kuwapisha mafundi kuendelea na kazi ya matengenezo.
“Waheshimiwa wajumbe kutokana na khitolafu ya umeme katika ukumbi wetu huu naomba kuakhirisha kikao hiki hadi hapo jioni ili tutoe nafasi kwa mafundi waliofika hapa kuja kututengenezea umeme kwa sababu jenereta lililowachwa haliwezi kutumalizia shughuli yetu hii muhimu” alisema Spika.
Hata hivyo wajumbe wa baraza la wawakilishi walionekana kutoka wakiwa na furaha baada ya kusikia kikao hicho kimeakhirishwa na waliendelea jioni baada ya matengenezo hayo kufanywa na wataalamu na mafundi kutoka Shirika la Umeme la Zanzibar (ZECO).
Ukumbi wa baraza la wawakilishi umejengwa kwa ufadhili wa Sheikh Ali Yussuf wa Saudi Arabia na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar lakini ukumbi huo umekuwa na khitilafu za mara kwa mara katika mitambo yake ya umeme, vipaza sauti na hata baadhi ya jengi hilo limekuwa kilivuja maji.
Afisa mmoja wa baraza hilo aliliambia Mwananchi kwamba ujenzi wa jengo hilo haukuwa mzuri aktika ramani yake kutokana na kuwa mafunzi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) wameshindwa kuona njia na paipu za kupitishia maji machafu na hivyo kuvuja kwa maji kumeshindikana licha ya juhudi kadhaa kufanywa na wataalamu wa ZAWA kujaribu kutaka kufanya marekebisho njia hizo za maji ndani ya jengo hilo.
“Jengo hili tokea limejengwa kuna matatizo mengi si unakumbuka wawakkilishi wakilalamikia vipaza sauti havisikiki na sasa umeme una matatizo lakini pia kuna tatizo la maji hapa wamekuja wafundi na wataalamu wengi sana lakini wameshindwa kuona paipi hawajui zimefukiwa au zimezamishwa wapi kwa hivyo maji yanamwagika na hayana pa kutokea na wale waliojenga wala hawapo sasa sijui tena serikali itafanyaje” alisema Afisa mmoja wa baraza la wawakilishi.

No comments :

Post a Comment