zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, March 15, 2013

Muhubiri mbaroni kwa uchochezi


Na Suleiman Abeid, Shinyanga 

MUHUBIRI wa dini ya Kikristo, mkazi wa Kigogo, Dar es Salaam, Damian Ndhimbo (35), juzi alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Maswa, mkoani Simiyu, akituhumiwa kusambaza nyaraka mbalimbali zinazodaiwa kuwa za uchochezi.

Nyaraka hizo zinadaiwa kupinga kitendo cha Waislamu kuendelea kuchinja nyama kwa ajili ya kitoweo.

Mbele ya Hakimu Thomson Mtani, Mwendesha Mashtaka wa mahakama hiyo, Kiduadi Karinga, alidai mshtakiwa alikamatwa
Machi 8 mwaka huu, saa 12 jioni, akiwa ndani ya Kanisa la
Katoliki Parokia ya Nyalikungu akitoa mahubiri ambayo
yangeweza kusababisha uchochezi.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, mbali ya kutoa lugha ya uchochezi mshtakiwa pia alikamatwa na CD za video na nyaraka za kupinga suala la uchinjaji kwa Waislamu.

Karinga alisema vitu hivyo vingeweza kusababisha uvunjifu wa
amani miongoni mwa waumini wa dhehebu la Kikristo na Kiislamu.

Hata hivyo, mshtakiwa alikana mashtaka hayo na kesi yake kuahirishwa hadi Machi 22 mwaka huu itakapotajwa tena
na yuko nje kwa dhamana.

Chanzo: Majira

No comments :

Post a Comment