Na Suleiman Abeid, Shinyanga
MUHUBIRI wa dini ya Kikristo, mkazi wa Kigogo, Dar es Salaam, Damian Ndhimbo (35), juzi alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Maswa, mkoani Simiyu, akituhumiwa kusambaza nyaraka mbalimbali zinazodaiwa kuwa za uchochezi.
Nyaraka hizo zinadaiwa kupinga kitendo cha Waislamu kuendelea kuchinja nyama kwa ajili ya kitoweo.
Mbele ya Hakimu Thomson Mtani, Mwendesha Mashtaka wa mahakama hiyo, Kiduadi Karinga, alidai mshtakiwa alikamatwa
Machi 8 mwaka huu, saa 12 jioni, akiwa ndani ya Kanisa la
Katoliki Parokia ya Nyalikungu akitoa mahubiri ambayo
yangeweza kusababisha uchochezi.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, mbali ya kutoa lugha ya uchochezi mshtakiwa pia alikamatwa na CD za video na nyaraka za kupinga suala la uchinjaji kwa Waislamu.
Karinga alisema vitu hivyo vingeweza kusababisha uvunjifu wa
amani miongoni mwa waumini wa dhehebu la Kikristo na Kiislamu.
Hata hivyo, mshtakiwa alikana mashtaka hayo na kesi yake kuahirishwa hadi Machi 22 mwaka huu itakapotajwa tena
na yuko nje kwa dhamana.
Chanzo: Majira
No comments :
Post a Comment