zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, March 30, 2013

Rais Kikwete awaongoza waombolezaji kuaga mwili wa mbunge


NA DANIEL MKATE

30th March 2013


Rais Dk.Jakaya Kikwete akiwa na viongozi wengine wa kitaifa wakihudhuria hitma ya Mbunge wa Chambani (CUF), Marehemu Salim Hemed Khamis kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam jana.
Rais Jakaya Kikwete, jana aliwaongoza waombolezaji kuaga mwili wa Mbunge wa Chambani (CUF), Salimu Hemed Khamis, katika viwanja vya Kamrijee Jijini Dar es Salaam.

Marehemu Khamis (62), alifariki juzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, baada ya kuanguka ghafla katika ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam wakati wa vikao vya kamati vikiendelea Jumatano iliyopita.

Kikwete aliwaongoza wabunge, viongozi wa vyama vya siasa na wananchi mbalimbali katika kuaga mwili wa marehemu Khamis, huku Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akiwa miongoni mwao.

Akizungumza baada ya kuuga mwili wa mbunge huyo, Spika wa Bunge la Tanzania, Anne Makinda, alisema Bunge limepata pigo kwa kuondokewa kiongozi makini ambaye alikuwa akiifahamu siasa na mtu makini.


“Marehemu alikuwa kiongozi makini kwa wenzake, mcheshi, mstaarabu na mjenga hoja…ni pigo kwa taifa kutokana na kumpoteza mtu aliyekuwa akiifahamu ipasavyo siasa,” alisema Makinda.

Na Katibu Mkuu wa Chadema, Wilbroad Slaa, alisema yeye pamoja na chama chake wamepokea kwa mshituko kifo cha mbunge Khamis.

Slaa alisema Khamis ametangulia wakati akiwa bado anahitajika kuipagania nchi yake katika masuala mbalimbali ya kitaifa, na pia alikuwa mstari wa mbele kushiriki kwenye mambo mbalimbali ya kijamii.

“Alikuwa rafiki yangu wa karibu, lakini kilichobaki sasa ni kumkumbuka katika utendaji wake wa kazi ili waliobaki waweze kuiga kizuri alichoacha,” alisema Slaa.

Akizungumzia salamu toka chama cha CUF, Naibu Katibu Mkuu, Julius Mtatiro alisema marehemu  alikuwa mstari wa mbele katika vikao vya usuluhishi hususani katika chama chake.

Aidha, Mtatiro alisema marehemu Khamis licha ya kuwa mtaalamu wa kilimo, pia alikuwa mtafiti wa siasa Tanzania Bara na Visiwani.

Hata hivyo, alisema CUF kimepata pigo baada ya kupokea kwa masikitiko na mshituko taarifa za kifo cha mbunge huyo ambaye alikuwa mstari wa mbele katika masuala ya upatanishi, usuluhishi na ushauri ndani ya chama chake pamoja na jimboni kwake.

Spika Makinda aliwaongoza wabunge 34 wa bunge la Jamhuri katika maziko ya marehemu Khamis aliyezikwa jana huko Chambani, Pemba.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment