Na Salome Kitomary
1st April 2013
(1).jpg)
Waziri Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Edward Lowassa, alitoa kauli ya kupitishwa kwa bajeti hiyo mwishoni mwa wiki, wakati akihairisha kikao cha kamati hiyo, kutokana na msiba wa mjumbe wa kamati hiyo, Mbunge wa Chambani (CUF), Salim Hemed Khamis, aliyefariki Alhamisi.
“Pamoja na msiba uliotupata, lakini natamka bajeti ya wizara hii imepitishwa kwa ajili ya vitabu vya Hazina, lakini tutaipitia kipengele kwa kipengele tutakapokutana mkoani Dodoma,” alisema Lowassa.
Awali, wajumbe wa kamati hiyo, walitaka kuwajua ni kwanini vikao vya bunge hilo havifanyiki nchini na kusikia vikiendelea kwenye nchi za wengine na kuwataka wabunge hao kuhakikisha vikao hivyo vinafanyika nchini.
CHANZO: NIPASHE
No comments :
Post a Comment