Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, May 10, 2013

Waingereza kuja kufundisha Kiingereza

NA MWANDISHI WETU

10th May 2013


Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa.
Wanafunzi wa ngazi mbalimbali ikiwemo vyuo vya walimu nchini, watanufaika na ujio wa wataalamu wa elimu kutoka nje kufundisha lugha ya Kiingereza.

Wataamu hao kutoka Uingereza watakuja nchini kufutia mradi wa mafunzo ya lugha ya Kingereza unaofadhiliwa na Taasisi ya elimu ya kingereza (British Council), VSO  kwa kushirikiana na serikali za uingereza na Tanzania.

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, wakati wa uzindizi wa mradi huo unaojulikana kama Mradi wa Uboreshaji wa Elimu (EUIP-T ELT) unaolenga pamoja na mambo mengine, nyanja ya mafunzo ya lugha ya Kingereza.

“Hii ni moja kati ya hatua ambazo wizara  imelenga kuzitekeleza ili kuboresha suala la elimu nchini, hivi sasa tunazo shule nyingi, lakini bado tumekuwa na changamoto katika suala zima la kuiboresha elimu yetu ili kukidhi viwango,” alisema.
Waziri Kawambwa alieleza kuwa mradi huo utatekelezwa kwa miaka minne na utagharimu fedha za  Paundi milioni 60 (Sh. bilioni 149).

Alifafanua kuwa mradi huo unalenga kuwanufaisha wanafunzi wa sekondari 700,000, wa shule za msingi  35,000, walimu wanafunzi  70,000; wakufunzi 1,650, wakuu wa taaluma 510, vyuo vya serikali 34 na wakaguzi 54.

Kwa upande wake, Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Kingereza (British Council), Sally Robinson, alieleza kuwa mradi huo unalenga kuwaandaa walimu pamoja na wanafunzi, ili wajue vyema lungha ya Kingereza katika kujifunza na vilevile kuwafundisha wengine.

“Kutokana na ushindani wa soko huria na mwingiliano wa kimawasiliano, sisi tumedhamiria kwa dhati kuboresha elimu ya Tanzania hususani katika kutoa mafunzo ya lugha ya Kingereza yenye kuzingatia viwango na ubora,” alisema.

Mwakilishi wa serikali ya Uingereza, Liz Tayler, alisema  Uingereza itahakikisha inashirikiana kikamilifu na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kuwaleta wataalamu wa lugha hiyo, msaada wa kifedha pamoja na zana za kazi.

“Sisi tunatoa walimu wenye sifa  kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wanafunzi wa vyuo vya ualimu wenye sifa,” alisema.

Waziri Kawambwa alisisitiza kwamba jamii itambue kuwa wahitimu wa kidato cha nne wa mwaka jana ambao matokeo yao yamefutwa, hawatarudia mtihani wala mtihani kusahihishwa upya kama inavyodhaniwa na wengi, isipokuwa kinachofanyiaka ni kubadilisha utaratibu wa madaraja uliotumika katika kupanga matokeo.

 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment