Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, October 10, 2013

CRDB BANK YAFANYA HAFLA FUPI UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON, DC NCHINI MAREKANI

Mhe. Balozi Liberata Mulaula katika picha ya pamoja
 na mkurugenzi mkuu wa CRDB Bank Dkt. Charles Kimei
 wakati wageni wakiingia kwenye hafla fupi iliyoandaliwa
 na CRDB kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani
 kwa ajili ya kutangaza huduma mpya za kibenki
 kwa ajili ya Diaspora na maboresho ya huduma ya Tanzanite.

Waziri wa Fedha na Uchumi Dkt. William Mgimwa akiingia
 kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani 
kulikofanyika hafla fupi iliyoandaliwa na CRDB Bank 
Jumatano Oct 9, 2013 kwa ajili ya kutambulisha huduma
 mpya za Benki hiyo kwa ajili ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi.

Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwatamburisha 
waheshimiwa wageni kwa baadhi ya Watanzania 
walofika kusikiliza huduma mpya za Benki ya CRDB
 kwa ajili ya Diaspora na maboresho ya huduma ya
 Tanzanite na baadae kumkaribisha mkurugenzi 
mkuu wa CRDB Bank Dkt. Charles Kimei kuongea 
na WanDMV kwa niaba ya WanaDiaspora.

Mkurugenzi mkuu wa CRDB Bank, Dkt Charles Kimei akielezea
 huduma hizo mpya ambazo ni JIJENGE (Mortgage Finance) 
na FAHARI HUDUMA (Argent Banking) na pia alielezea
 maboresho ya hudma ya Tanzanite ikiwemo mteja
 anapofkisha kiasi fulani cha pesa kwenye akaunti yake
 hakutakuwa na makato ya aina yeyote yatakayokatwa kila mwezi.

Waziri wa Fedha na Uchumi Dkt. William Mgimwa
 akiongea machache na kuwaambia wanaDMV 
wajisikie wapo Tanzania na salama kwani
 amekuja na ujumbe mzito unaowakilisha Bara 
na visiwani na baadae kumshukuru Mhe. Balozi 
Mulamula kwa makaribisho mazuri na CRDB Bank 
kwa kuandaa hafla hiyo fupi iliyofanyikia Ubalozi wa
 Tanzania nchini Marekani Jumatano Oct 9, 2013 jioni.

Waziri wa Fedha na Uchumi akiongoza ujumbe 
wake kwenye chakula cha jioni.

Duputy Governor Economic & Financial Policies
 Dkt. Natu El- maamry Mwamba akijiatia chakula cha jioni.


Mhe. Balozi Liberata Mulamula nae akijipatia chakula cha jioni.

Kulia ni Waziri wa Fedha na Uchumi Zanzaibar Mhe. Yussuf Mzee akibadilishana mawili matatu toka kushoto ni Mariam
 Mkama, Love Maganga na Tully Esther Mwambapa 
ambaye nia Director of Marketing, Reserch and 
Customer Service wa CRDB Bank.

Mkurugenzi mkuu wa TRA Harry Kitilya (kati) 
akibadilishana mawili matatu na Mwambata 
wa Jeshi Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani 
Colonel Adolph Mutta (kushoto) na Afisa 
Ubalozi Dkt. Switebert Mkama.
kwa picha zaidi bofya soma zaidi















































Mshereheshaji Afisa Ubalozi Suleiman Saleh
Juu na chini wadau wakifuatilia mawili matatu 
kutoka kwa watoa hutuba.

Wageni waheshimiwa wakipata chakula cha jioni.
Juu na chini ni Warizi wa Fedha na Uchumi na 
ujumbe wake wakibadilishana mawili matatu 
na Balozi  Liberata Mulamula baada ya 
kumaliza kupata chakula cha jioni kwenye
 hafla fupi iliyoandaliwa na CRDB Bank 
kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani.
Balozi wa Tanzania nchini Marekani akiwaaga wageni
 wake mara lipomalizika hafla hiyo picha 
Mhe. Liberata Mulamula akiagana na Gavana
 wa Bank Of Tanzania Prof. Beno. Ndulu 
kushoto ni Baraka Munisi ambaye ni
 Mortgage Finance Specialist.
Baraka Munisi (kushoto akiongea jambo 
na Prof Benno Ndulu huku Baraka Daudi(kati) ski sikiliza.

No comments :

Post a Comment