AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, December 3, 2013

Tanzania inafanya vizuri uwekezaji

NA MWANDISHI WETU

2nd December 2013


Waziri wa Nchi Ofisi ya wa Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk. Mary Nagu wa pili kulia, akizindua ripoti ya Uwekezaji Tanzania mwaka 2012, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Juliet Kairuki na kushoto ni Naibu Gavana wa Benki Kuu (BoT), Dk. Natu Mwamba.
Tanzania imeendelea kufanya vizuri katika sekta  ya uwekezaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa na ajira kwa Watanzania.

Ripoti ya Uwekezaji Tanzania ya mwaka 2012 inaonyesha kuwa uwekezaji katika sekta nyingi za uchumi zimefanya vizuri isipokuwa sekta ya kilimo.

Akizindua ripoti hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita, Waziri  wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji),  Dk. Mary Nagu, alisema serikali bado inaendelea kuyafanyia kazi maeneo mbalimbali ili kuboresha zaidi mazingira ya uwekezaji nchini.

 “Kazi kubwa iliyopo mbele yetu ni kuongeza kasi ya uwekezaji katika sekta za madini na gesi ili kuisaidia nchi kupata faida zaidi na kutumia fursa hiyo kujenga miundombinu katika sekta ya ya Kilimo ili nayo iweze kuvutia uwekezaji zaidi,” alisema.

Alisema ripoti hiyo imeonyesha kuwa mazingira ya uwekezaji nchini ni mazuri na yanavutia wawekezaji kuja kuwekeza.

Nagu alisema katika mazingira hayo serikali ingependa kuona ongezeko hilo la uwekezaji linaenda sambambana na maendeleo ya uchumi wa watanzania wa kawaida.

Ripoti hiyo imekuja baada ya Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Ofisi ya Taifa Takwimu (NBS), kufanya utafiti ambao umekuja na majibu yaliyolenga kuonyesha hali halisi na changamoto zilizopo ili kupata fursa ya kufanya maboresha mazingira ya uwekezaji nchini.

Dkt.Nagu alisema kuwa  serikali itatumia ripoti hiyo na kuhakikisha inakuwa ni sehemu ya kufanyia maboresho ya sera ya uwekezaji ambayo itaweka mazingira bora zaidi ya uwekezaji  nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa TIC),  Juliet Kairuki alisema utafiti huo uliohusisha kampuni zilizowekeza Tanzania Bara na Visiwani utatumika katika kupanga mikakati zaidi ya kuongeza uwekezaji.

Naye Mkurugenzi wa Mkuu wa NBS, Dk. Albina Chuwa, alisema utafiti huo umefanyika kwa kufuta vigezo vya Ofisi ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa .


 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment