dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, April 23, 2014

Maalim Seif ashambuliwa - Adaiwa kuiba waraka

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad

Utetezi wa muundo wa Muungano wa serikali mbili katika mjadala wa katiba jana ulichukua sura mpya kwa kuelekeza mashambulizi mengi dhidi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad kuwa ni mtu kigeugeua sawa na kinyonga.

Mashambulizi hayo yalianza asubuhi wakati Mohammed Seif Khatib alijadili sura ya kwanza na ya sita ya rasimu ya katiba, akimwelezea Maalim Seif kuwa ni mtu anayebadilika kama kinyonga, kiasi cha kudirikia kuiba nyaraka Ikulu iliku kuulinda Muungano wa serikali mbili, lakini sasa amegeuka na kusaka serikali tatu na Muungano wa mkataba.

Khatib alisema kuwa Maalim Seif aliwachongea viongozi wa Zanzibar, akiwamo Rais wa awamu ya pili, Abood Jumbe, ili kutetea Muungano wa serikali mbili.

Mbali na Jumbe, wengine wanaodaiwa kuchongewa na Maalim Seif mwaka 1984, ni Waziri Kiongozi mstaafu, Ramadhani Haji Fakhi, na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Wolfgang Dourado, wa wakati huo.

Alisema Maalim Seif aliwashitaki viongozi hao kwa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye mkutano wa Kamati Kuu (CC) ya chama hicho mwaka huo akidai kwamba walitaka kubadilisha katiba na kuwa na Muungano wa serikali tatu.

Khatib alisema Maalim Seif alidai kuwa Dourado alikuwa anasafiri kati ya London na Zanzibar ili kukashifu viongozi wa Muungano na kuwachochea watu wauchukie kuwa siyo wa halali.
Alisema Maalim Seif alidai kuwa kwa safari hizo Dourado aliangamiza fedha za kigeni na kuhoji alipata wapi jeuri ya kuwasemea Wazanzibari.

Khatib alimnukuu Maalim Seif akisema kuwa viongozi hao walifanya vitendo vya uhaini na kutaka Halmashauri Kuu (Nec) iwahukumu.

Alinukuu kauli za Maalim Seif aliyesema: “Suala la serikali tatu limepewa uzito mkubwa katika waraka na linachochewa na Makamu Jumbe.”

Aidha, alimtuhumu Maalim Seif kuwa ni kiongozi wa ajabu aliyediriki kuiba waraka wa siri kwenye Ikulu ya Zanzibar na kuungama kuwa alifanya hivyo kama alivyonukuliwa kwenye kitabu cha Profesa Issa Shivji.

Khatib alisema Maalim Seif aliiba waraka huo kwenye shubaka (droo) ya Rais Ikulu ili kutetea muundo wa serikali mbili.

Alimfananisha Maalim Seif na kinyonga, ambaye mwaka 1984 alitetea serikali mbili baada ya kutimuliwa CCM Mei 13, 1988, alitaka serikali tatu na mwaka jana akaibuka na Muungano wa mkataba.

DK. MWAKYEMBE AONGEZA MASHAMBULIZI
Dk. Harrison Mwakyembe naye aliendeleza mashambulizi dhidi ya Maalim Seif alipomkariri katika moja ya hotuba zake akisema:

“Naamini maslahi ya Zanzibar yana uhakika zaidi katika Muungano huu, ambao umesaidia kuzuia machafuko na kuepusha vifo vya watu wasio na hatia Zanzibar na kwamba, ndiyo uliodumisha amani.”

Alimnukuu akiahidi: “Nitaandelea kudumisha Muungano na kuyatetea maslahi ya Zanzibar.”

Dk. Mwakyembe alisema Maalim Seif licha ya kuteta serikali mbili katika mfumo wa Muungano, aliwahi kudai kuwa kero zilizoko siyo za msingi.

Naye Hamad Rashid Mohammed alitumia fursa ya jana kuweka wazi walivyohusika yeye na Maalim Seif kupeleka waraka wa Jume kwa Mwalimu Nyerere baada ya kuongea na Waziri Mkuu, Edward Sokoine.

Hamad alisema kuwa walimfuata Mwalimu Butiama baada ya kusoma waraka wa Jumbe, aliitisha kikao cha Kamati Kuu lakini mwafaka haukupatikana ikabidi Nec iitishwe na mwishowe maamuzi ya kuvuliwa madaraka Jumbe yalifikiwa.

Alisema kuwa Ali Hassan Mwinyi aliagizwa kugombea urais Zanzibar na alitakiwa amteue Maalim Seif kuwa Waziri Kiongozi.

Alimshutumua Maalim Seif kwa usaliti na kwamba anajitwisha Uzanzibari kuliko Wazanzibari wengine, lakini kinachomsumbua ni kutaka madaraka tu kwani alimfaia vitimbi pia Mzee Abdul Wakili, ambaye akiteuliwa kugombea urais baada ya Mwinyi kuwa Rais wa Tanzania.
CHANZO: NIPASHE

1 comment :

  1. Nikweli na alifanya hivo kwa kuwa sikuzili alikuwa ni muumini waccm, illikuwa hakiyake kuulinda muungano kama hawa ccm wasasa

    ReplyDelete