na
Wana-blog wote,
Kama desturi yetu, tarehe 31 December, 2014, Zanzibar Ni Kwetu (ZNP) baada ya kukutakieni kheri za mwaka mpya itakula kiapo kwa mara ya nne mfululizo, kuwa tutaendelea kuulinda
Muungano pamoja na matunda yake yote kwa nguvu zetu zote za kalamu.
Suala kubwa lakujiuliza ni kuwa, Muungano gani huo
ambao Zanzibar Ni Kwetu itaapa kuulinda kwa mwaka mzima ujao wa 2015?
Ni Muungano ule wa Mzee Mwanakijiji alietaka kutupa bilioni
400 (TShs) ili tutoke na tumuachie jina la Tanzania
baada ya yeye kukwapuwa bilioni 306 in a day-light robbery?
Au ni Muungano ule wa wananchi ambao wameoza na wanashindwa
kuanzisha African Spring (civil disobedience) ili kudai pesa zilizoporwa
zirejeshwe kwenye Akaunti ya Escrow?
Au ni Muungano ule wa mtu mmoja anaeitwa Mzee
Vijisenti ambae hata akiwaibia watu mchana anaogopwa hata na mkuu wa nchi kuambiwa
arejeshe pesa alizopora?
Au ni Muungano ule ambao Rais wake anashindwa
kuzidai zirejeshwe pesa zilizoporwa na wezi nchini, kwasababu na
yeye Rais itabidi arejeshe?
Ni Muungano gani huo ambao Zanzibar Ni Kwetu itaapa
kuulinda?
Tega sikio!
No comments :
Post a Comment