Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, June 7, 2015

Maalim SeIf aahidi kuanzisha Wizara ya Mafuta na Gesi akitinga Ikulu

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Sharif Hamad
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Sharif Hamad,  anakusudia kuanzisha Wizara ya Mafuta na Gesi, ikiwa ni vipaumbele vyake akichaguliwa kuiongoza Zanzibar.

Hamad ambaye ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, ambaye CUF imemteua kuwa mgombea wa urais wa Zanzibar kwenye  uchaguzi mkuu wa Oktoba, ameeleza hayo jana.

Alikuwa akihutubia mkutano wa  mapokezi ya mgombea huyo.
Sambamba na hilo aliahidi kuwa endapo atachaguliwa kuiongoza Zanzibar, atahakikisha kuwa Zanzibar inakuwa na shirika  la ndege ndani ya kipindi cha mwaka mmoja ili kurahisisha safari na shughuli za kibiashara ikiwamo utalii.

Aliahidi kuitangaza  Zanzibar kuwa bandari huru, sambamba na kujenga bandari mpya itakayotoa huduma bora kwa mwambao wa Afrika Mashariki.
Alisema Zanzibar inazo fursa nyingi za kuweza kunyanyua kipato cha wananchi na kwamba ataweka kipaumbele katika kuziibua na kuziendeleza.

Alisema katika kujenga mazingira bora ya uwekezaji, ataisimamia ipasavyo mamlaka ya vitega uchumi ili kuondosha vizingiti vinavyokwamisha uwekezaji.

Alifahamisha kuwa wapo wafanyabiashara wengi wa ndani na nje ya nchi wenye nia ya kuwekeza miradi mikubwa ya kiuchumi, lakini wamekwamishwa  jambo ambalo ameahidi kulishughulikia mara akiingia madarakani.

Mapema akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti wa CUF Taifa Profesa  Ibrahim Lipumba, alisema Baraza Kuu la Uongozi la CUF limeshawishika kumuidhinisha Hamad kuwa mgombea urais wa Zanzibar, kutokana na uwezo na nia ya dhati ya kuwatumikia Wazanzibari.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

No comments :

Post a Comment