.jpg)
Hamad ambaye ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, ambaye CUF imemteua kuwa mgombea wa urais wa Zanzibar kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba, ameeleza hayo jana.
Alikuwa akihutubia mkutano wa mapokezi ya mgombea huyo.
Sambamba na hilo aliahidi kuwa endapo atachaguliwa kuiongoza Zanzibar, atahakikisha kuwa Zanzibar inakuwa na shirika la ndege ndani ya kipindi cha mwaka mmoja ili kurahisisha safari na shughuli za kibiashara ikiwamo utalii.
Aliahidi kuitangaza Zanzibar kuwa bandari huru, sambamba na kujenga bandari mpya itakayotoa huduma bora kwa mwambao wa Afrika Mashariki.
Alisema Zanzibar inazo fursa nyingi za kuweza kunyanyua kipato cha wananchi na kwamba ataweka kipaumbele katika kuziibua na kuziendeleza.
Alisema katika kujenga mazingira bora ya uwekezaji, ataisimamia ipasavyo mamlaka ya vitega uchumi ili kuondosha vizingiti vinavyokwamisha uwekezaji.
Alifahamisha kuwa wapo wafanyabiashara wengi wa ndani na nje ya nchi wenye nia ya kuwekeza miradi mikubwa ya kiuchumi, lakini wamekwamishwa jambo ambalo ameahidi kulishughulikia mara akiingia madarakani.
Mapema akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti wa CUF Taifa Profesa Ibrahim Lipumba, alisema Baraza Kuu la Uongozi la CUF limeshawishika kumuidhinisha Hamad kuwa mgombea urais wa Zanzibar, kutokana na uwezo na nia ya dhati ya kuwatumikia Wazanzibari.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

No comments :
Post a Comment