dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, October 6, 2015

M/kiti CWT aliyepanda jukwaani kampeni za Lowassa ashtakiwa.

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA).
Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Chato, Lucas Michael, maarufu Masai kupanda jukwaani na kuzungumza  kwenye mkutano wa kampeni za mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa na kuilalamikia serikali kushindwa kuwarejesha makwao walimu waliostaafu, kulipa madai ya walimu, pamoja na kutopandisha madaraja kwa wakati, serikali imemshitaki.
 
Katika madai yake, Michael pia alidai kusikitishwa na kitendo cha serikali ya wilaya ya Chato kuwaandama baadhi ya walimu wanaoonekana kuunga mkono vyama vya upinzani, huku wanaokiunga mkono CCM wakionekana wako sahihi, kitendo alichodai ni ukandamizwaji wa demokrasia. 
 
Mwenyekiti huyo wa CWT alihudhuria mkutano wa kampeni za mgombea huyo wa urais alipofika wilayani Chato Septemba 19, mwaka huu, baada ya kupokea mwaliko wa Chadema wilayani humo akiwa kama mdau wa elimu.
 
Kufuatia hatua hiyo, mwenyekiti huyo wa CWT wilaya ya Chato ameshitakiwa kwenye Tume ya Utumishi wa Umma Idara ya Utumishi wa Walimu wilayani hapa, kwa madai ya kukiuka maadili na taratibu za utumishi, kanuni namba 65 (1) na kutakiwa kujieleza.
 
Hati ya shitaka ambayo imesainiwa na Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Frank Angus, Septemba 22, mwaka huu, inadai kuwa mwalimu huyo alitenda kosa la kujihusisha na masuala ya kisiasa, kuchukua taarifa za kiutumishi na kuzisema kwenye mkutano wa kisiasa pamoja na kutumia nafasi yake akiwa mtumishi wa Umma kumnadi mgombea urais wakati wa kampeni.
 
Akizungumza na Nipashe mjini hapa jana, Michael alithibitisha  kupokea hati ya shitaka hilo. Hata hivyo, alisema hakuhusika kufanya kampeni za mgombea urais kupitia Chadema isipokuwa alisimama kuzungumzia malalamiko ya walimu wa wilaya ya Chato.
 
Alidai alialikwa kuhudhuria mkutano huo wa kampeni kupitia barua ya Chadema yenye kumbu kumbu namba Chadema /CHT/G/M/1/015 na ana amini alitimiza wajibu wake kwa mujibu wa katiba ya CWT.
 
Naye Katibu wa Chadema Wilaya ya Chato, Mange Ludomya, alisema mwalimu huyo alialikwa kwenye mkutano huo kama mwenyekiti wa CWT ambacho ni wadau wa elimu nchini kutokana na umuhimu wake, ikizingatiwa kwamba kipaumbele cha chama hicho iwapo kitapewa ridhaa ya kuongoza nchi ni elimu.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment