Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, December 23, 2015

Waziri Mkuu Majaliwa aahidi daraja Mto Mbwemkuru kukamilika haraka

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Waziri mkuu Kassim Majaliwa amesema ujenzi wa daraja la Mto Mbwemkuru lililoko katika barabara ya kutoka Chikwale hadi Liwale litakamilika haraka kwa sababu ni kiungo muhimu kwa wakazi wa eneo hilo.
 
Amlitoa ahadi hiyo wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Nangurugai, kata ya Mbwemkuru, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi, ambako alikwenda kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mbunge wao.
 
Waziri Mkuu alikuwa akijibu hoja za Diwani wa Nangurugai, Selemani Likuche, aliyetoa ombi la kutengenezwa kwa daraja hilo kutokana na kukata mawasiliano baina ya kijiji hicho na wilaya ya Liwale. 
 
Pia aliomba wapatiwe dawa na watumishi kwenye zahanati yao.
 
Akijibu hoja hizo, Waziri Mkuu alisema kazi ya ujenzi wa daraja hilo itakamilishwa haraka. Pia aliitaka Halmashauri ya Ruangwa isimamie uboreshaji wa barabara ya kutoka Nangurugai hadi Chikwale yenye urefu wa kilomita 35 kwa sababu ni muhimu kwa kusafirisha mazao katika eneo hilo.
 
“Hili eneo ni maarufu kwa zao la ufuta, kwa maana hiyo linaongeza pia mapato ya halmashauri, simamieni hii barabara ili wananchi wasisumbuke kuuza mazao yao,” alisema.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa, Nicholas Kombe, alisema milingoti  ya daraja hilo ilikwishajengwa na kinachosubiri ni kupokea vyuma vya kutandaza juu ya daraja.
 
Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa dawa kwenye zahanati yao, Majaliwa alisema ameshazungumza na Mganga Mkuu wa wilaya hiyo ambaye amemhakikishia kuwa ameanza maboresho ya upatikanaji dawa katika zahanati zote.
 Kuhusu tatizo la watumishi wa sekta ya afya, aliahidi kuwa watapatikana katika muda mfupi.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment