zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, January 30, 2016

Magufuli awaondoa Chagonja na Mtweve polisi

Rais wa John Magufuli.
Rais wa John Magufuli amemwondoa Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja na kumteua kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Katavi.
Katika mabadiliko hayo pia Magufuli amemwondoa Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi hilo, Clodwing Mtweve na kumteua kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza.
Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, wateule hao wanakwenda kujaza nafasi za Makatibu Tawala wa mikoa hiyo.
Tarifa hiyo ilisema Clodwing Mtweve amekwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Faisal Issa ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Sefue alisema Chagonja anakwenda Katavi kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Madeni Kipande ambaye uteuzi wake ulitenguliwa pia.
Aidha, Balozi Sefue alisema Rais Magufuli amewateua Makamishna hao wa Polisi kama alivyowateua Majenerali wa Jeshi la Wananchi Tanzania kuwa Makatibu Wakuu wa Wizara, kwa lengo la kujenga nidhamu katika utumishi wa umma.
Makamishna Mtweve, Chagonja na Mahadhi Juma Maalim ambaye ameteuliwa kuwa Balozi Mpya wa Kuwait, wataapishwa leo Jumamosi asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment