zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, March 5, 2016

Serikali yashtuka bei ya saruji ya Dangote mkoani Mtwara

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Serikali imeahidi kuwaita viongozi wa kiwanda cha saruji cha kampuni ya Dangote Group kilichopo mkoani hapa, kuwataka waeleze sababu zilizosababisha saruji inayozalishwa hapo kuuzwa bei kubwa mkoani Mtwara huku Dar es Salaam ikiuzwa kwa bei ya chini.
 
Kauli hiyo ilitolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokuwa akiwahutubia wakazi wa Mtwara katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Mashujaa.
 
Waziri Mkuu alifanya ziara mkoani humu kwa lengo la kuwapa pole waathirika wa mafuriko pamoja na kutembelea baadhi ya maeneo ikiwa ni pamoja na Bandari na kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba.
 
Majaliwa alisema serikali inahamasisha ujenzi wa viwanda vingi zaidi ili kutoa mwanya kwa wananchi kupata ajira na kwa kuanzia jitihada zimeanza kuonekana katika viwanda vya saruji ambavyo uzalishaji umeanza.Hata hivyo, alisema serikali haijaridhishwa na bei ya bidhaa hiyo iliyoanza kuingizwa sokoni hivi karibuni kutoka katika kiwanda cha Dangote.
 
“Tunahangaika na bei, hatujapata bado vizuri bei ya Dangote, naambiwa saruji Mtwara ni Sh. 13,500, lakini saruji hiyo hiyo ukienda Dar es Salaam inauzwa Sh. 11,000. Hili bado serikali itafuatilia..tutawaita tutawataka watupe maelezo sahihi, maana ya kuwa na kiwanda mahali ni pamoja na kupata bidhaa hiyo kwa bei nafuu. Kama Dangote anazalisha saruji halafu saruji hiyo hiyo Mtwara iuzwe Sh. 13,500 na Dar es Salaam Sh. 11,000, haieleweki,” alisema Waziri Mkuu.
 
Alisema serikali bado ina matumaini makubwa na uwapo wa viwanda hivyo kwa kuwanufaisha wananchi wanunue saruji kwa bei ya kawaida ili kila mmoja amudu kujenga nyumba imara kwa kutumia saruji.
 
Kuhusu ujenzi wa kiwanda cha mbolea ambacho mchakato wake unaendelea, alisema serikali itahakikisha inafanya mapitio ya mikataba ikiwa ni pamoja na kuwahimiza kuharakisha ujenzi huo ili wakulima waanze kutumia mbolea hiyo na wananchi watapata taarifa hizo kupitia viongozi wao.
 
Aidha, katika kuwaondoa hofu wananchi wa Mtwara juu ya ubovu wa miundombinu ya barabara, Waziri Mkuu alisema serikali imedhamiria kufungua milango ya mkoa huo kwenda nje ya mkoa huo na kuwa barabara ya uchumi ya Mtwara-Nanyamba-Tandahimba-Newala na Masasi, ipo kwenye mpango wa ujenzi kwa kiwango cha lami.
 
“Taratibu za awali za kutambua wanasema usanifu, tayari zimeshafanywa na wabunge hili ndilo jambo ambalo wamelisimamia kidete kwamba lazima barabara ile inajengwa kwa lami,” alisema.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment