dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, April 14, 2016

JPM, Salva Kiir, kusaini mkataba kuipokea Sudan Kusini

  • MWENYEKITI wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Rais John Magufuli na Rais Salva Kiir Mayardit wa Sudan Kusini, wanatarajia kusaini mkataba wa kuipokea nchi hiyo kuwa mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano ya EAC, Owora Richard Othieno, alisema katika taarifa yake juzi kwamba utiaji wa saini hiyo unatarajiwa kufanyika kesho (Ijumaa), jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano mkuu wa 17 wa kawaida wa wakuu wa EAC, uliofanyika Machi 2 mwaka huu, jijini Arusha, wakuu hao walipokea ripoti ya Baraza la Mawaziri kuhusu mazungumzo ya makubaliano yao ya kuipokea Sudan Kusini kama mwanachama mpya.

Owora alisema mkutano huo ulimpa kazi Rais Magufuli kusaini mkataba wa kuipokea rasmi Sudan Kusini.

No comments :

Post a Comment