dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, April 14, 2016

Ombaomba waanza kusombwa

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda

By Vicky Kimaro, Mwananchi 
Dar es Salaam. Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda limeanza kufanyiwa kazi baada ya karandinga kuanza kuwasomba ombaomba waliojaa katika maeneo mengi jijini hapa.
Makonda alitangaza kuanza kuwaondoa ombaomba hao juzi, huku akipiga marufuku wananchi kuwapa pesa kwa kuwa ndicho chanzo cha kuwapo kwao jijini hapa.
‘Mchakamchaka’ wa kuwaondoa watu hao ulianza juzi usiku katika maeneo ya Mnazi Mmoja, Samora na Kariakoo.
Mwananchi ilizunguka maeneo mbalimbali ambayo aghalabu ombaomba hupenda kukaa, lakini yalikuwa tupu.
Maeneo hayo ikiwamo barabara ya Morocco, Magomeni Usalama, Fire na Baridi hayakuwa na watu wa kundi hilo.
Mmoja wa ombaomba aliyekuwa na watoto wawili alipomuona mwandishi wa habari hizi katika maeneo ya Fire, alitimua mbio na kujificha pembeni mwa barabara, huku akisema: “Tumetoka Dodoma, hatutaki kurudi.”
Akizungumza na gazeti hili, Makonda alisema ikifika Jumatatu kama hawajajisalimisha Serikali itachukua hatua kali na kuwarudishwa walikotoka. “Kwanza ni kinyume cha sheria, pili ni hatari kwa maisha yao na watoto wanatakiwa warudi shule sasa,” alisema.
Kadhalika, operesheni hiyo licha ya timuatimua kuwakumba ombaomba, wapigadebe nao wameunganishwa katika kundi hilo kwa kuanza kuondolewa kwenye vituo vya mabasi.
Baadhi ya wapigadebe hao wamedai ni vigumu kwa Makonda kuwaondoa kwa kuwa wanachofanya ni kwa manufaa ya maisha yao na hawana pa kwenda.
Agizo la kutaka ombaomba wakamatwe na kuondokana na vitendo hivyo liliwahi kutolewa pia na waliowahi kuwa wakuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Yusuf Makamba, Abbas Kandoro na Said Mecky Sadiki. 

No comments :

Post a Comment