dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, April 15, 2016

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI-MKATABA SUDAN KUSINI NA COMMUNIQUETAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI-MKATABA SUDAN KUSINI NA COMMUNIQUE

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE, USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI, KIKANDA NA KIMATAIFA

Coat of Arms

Simu: 255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: nje@nje.go.tz
Barua pepe: gcu@nje.go.tz

Nukushi: 255-22-2116600

              

               20 KIVUKONI FRONT,
                          P.O. BOX 9000,
                 11466 DAR ES SALAAM,  
                                   Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Sudan Kusini yasaini rasmi Mkataba  wa kujiunga Jumuiya ya Afrika Mashariki

Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa pamoja na Mhe. Salva Kiir Mayardit, Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini wamesaini Mkataba wa kuiwezesha Jamhuri ya Sudan Kusini kuwa Mwanachama kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Tukio hilo la kihistoria limefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Aprili, 2016.

Akizungumza wakati wa haflya hiyo, Mhe. Dkt. Magufuli aliipongeza nchi hiyo na kusema kuwa anajivunia tukio hili la kihistoria kutokea wakati Tanzania ikiwa ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwamba ukurasa mpya wa ushirikiano na mahusiano na nchi hiyo umefunguliwa.

Aliongeza kuwa kihistoria  Sudan Kusini, imekuwa  na mahusiano ya karibu na nchi za Afrika Mashariki katika nyanja mbalimbali ikiwemo mwingiliano wa tamaduni, ushirikiano wa kibiashara na uchumi na ukaribu wa kijografia.  Aidha, alieleza kuwa kujiunga kwa Sudan Kusini kwenye EAC kunaifanya Jumuiya hii kuwa na soko kubwa lenye takriban watu milioni 160.


Vile vile Mhe. Rais Magufuli alisema kuwa ili Jumuiya ya Afrika Mashariki iweze kuwa na maendeleo endelevu suala la kudumisha amani ni la msingi, hivyo aliwahimiza Sudan Kusini kuendeleza juhudi kwenye mazungumzo ya amani.‘’Dhana ya Mtangamano ni kukuza biashara, uwekezaji na miundombinu ili kujiletea maendeleo endelevu katika Jumuiya yetu,  hivyo nahimiza  umuhimu wa nchi wanachama kudumisha amani ili kufikia malengo tuliyojiwekea ‘’ alisema Rais Magufuli.

Wakati huohuo, Rais Magufuli alimpongeza Rais Kiir kwa jitihada zake katika kuhakikisha nchi yake inajiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki haraka ambapo miezi minne baada ya nchi hiyo kupata uhuru iliwasilisha maombi ya kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki na miaka mitano imeweza kuwa mwanachama kamili wa Jumuiya hiyo.

Kwa upande wake, Rais Kiir alieleza kufurahishwa kwake na hatua iliyofikiwa na nchi yake ya kuwa mwanachama kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Aidha, alimshukuru Rais Magufuli na Marais wa Nchi zote wanachama kwa kuiunga mkono nchi yake kwa kauli moja.

Mhe. Kiir aliongeza kuwa uamuzi wa nchi yake wa kujiunga na Jumuiya ni wa dhati na kwamba una nia ya kuimarisha ushirikiano kwa manufaa ya wananchi wa Afrika Mashariki kwa ujumla, ambapo nchi yake imeshaanza kufanyia mabadiliko mifumo mbalimbali kwenye Serikali yake ili kuweza kushiriki kikamilifu katika hatua mbalimbali za mtangamano ikiwemo kuunda Wizara inayoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki.

‘’Hatimaye Sudan Kusini imerudi nyumbani. Jumuiya ya Afrika Mashariki ni sehemu sahihi kwa nchi yangu kwani Jumuiya ya Afrika Mashariki ni mtangamano unaoheshimika Afrika na Duniani kwa ujumla’’ alisisitiza Rais Kiir.

Pia, Rais Kiir alitangaza kufunguliwa rasmi kwa Ubalozi wa nchi yake hapa nchini na tayari amemteua Balozi Mariano Deng Ngor kuwa Balozi wa Sudan Kusini nchini Tanzania.

Awali akizungumza kabla ya kusainiwa kwa Mkataba huo, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga alisema kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki itashirikiana kwa karibu na Jumuiya ya Kimataifa kuhakikisha wananchi wa Sudan Kusini waliothirika na migogoro na kuikimbia nchi yao wanarejea kwa ajili ya kuendeleza nchi yao.

Jamhuri ya Sudan Kusini ilipata uhuru wake tarehe 09 Julai, 2011 na iliwasilisha maombi rasmi ya kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki tarehe 10 Novemba, 2011. Aidha, Tangazo la kukubaliwa kuwa Mwanachama wa EAC lilitangazwa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa  Mkutano wa 17 wa Wakuu wa Nchi wa EAC uliofanyika jijini Arusha mwezi Machi 2016.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa

Dar es Salaam, 15 Aprili, 2016



EAST AFRICAN COMMUNITY




COMMUNIQUÉ ON THE SIGNING CEREMONY OF THE TREATY OF ACCESSION OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN INTO THE EAST AFRICAN COMMUNITY




STATE HOUSE, DAR ES SALAAM, TANZANIA

15TH APRIL, 2016






EAC SECRETARIAT

ARUSHA, TANZANIA

APRIL 2016


SIGNING CEREMONY OF THE TREATY OF ACCESSION OF THE REPUBLIC OF
SOUTH SUDAN INTO THE EAST AFRICAN COMMUNITY

COMMUNIQUÉ



  1. THEIR EXCELLENCIES GENERAL SALVA KIIR MAYARDIT, PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN, AND DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND CHAIRPERSON OF THE EAST AFRICAN COMMUNITY SUMMIT OF HEADS OF STATE HAVE THIS FRIDAY THE 15TH OF APRIL 2016, SIGNED THE TREATY OF ACCESSION OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN INTO THE EAST AFRICAN COMMUNITY IN DAR ES SALAAM, TANZANIA. THE HEADS OF STATE MET AND SIGNED THE TREATY OF ACCESSION IN A WARM AND CORDIAL ATMOSPHERE.

  1. H.E. DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI WAS DESIGNATED ON 2ND MARCH, 2016 BY THE SUMMIT OF EAC HEADS OF STATE AT THEIR 17TH ORDINARY MEETING, ON ITS BEHALF, TO SIGN THE TREATY OF ACCESSION WITH H.E. GENERAL SALVA KIIR MAYARDIT, PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN
  2. H.E. DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI THANKED H.E. GENERAL SALVA KIIR MAYARDIT FOR TAKING THE INITIATIVE TO FORMALLY APPLY FOR MEMBERSHIP TO THE EAST AFRICAN COMMUNITY IN LESS THAN FOUR MONTHS AFTER THE COUNTRY ATTAINED INDEPENDENCE.

  1. THEIR EXCELLENCIES THE HEADS OF STATE NOTED THAT THE ENTRY OF SOUTH SUDAN INTO THE EAST AFRICAN COMMUNITY WAS FOR THE BENEFIT OF THE ENTIRE REGION.

  1. H.E. GENERAL SALVA KIIR MAYARDIT THANKED THE SUMMIT OF EAC HEADS OF STATE FOR AGREEING TO ADMIT THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN INTO THE EAST AFRICAN COMMUNITY.

  1. H.E. GENERAL SALVA KIIR MAYARDIT OBSERVED THAT THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN’S ADMISSION INTO THE EAST AFRICAN COMMUNITY WAS THE FULFILMENT OF A DREAM HELD BY THE COUNTRY’S FOREFATHERS MORE THAN FIFTY YEARS AGO, ADDING THAT IT MARKED A DECISIVE SHIFT IN THE COUNTRY’S FOREIGN AND ECONOMIC POLICY.

  1. H.E. DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI DIRECTED THE EAC SECRETARIAT TO URGENTLY DEVELOP A ROADMAP FOR FAST-TRACKING THE INTEGRATION OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN INTO THE ACTIVITIES, PROGRAMMES AND PROJECTS OF THE EAST AFRICAN COMMUNITY.


  1. H.E. GENERAL SALVA KIIR MAYARDIT, PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN, THANKED HIS EXCELLENCY DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND CHAIRPERSON OF THE EAC SUMMIT OF HEADS OF STATE, FOR THE WARM AND CORDIAL HOSPITALITY EXTENDED TO HIM AND HIS DELEGATION DURING THEIR STAY IN TANZANIA.


DONE AT DAR ES SALAAM, THIS 15TH DAY OF APRIL, 2016.



………………….............…....................

H.E. DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA; AND CHAIRPERSON, EAC SUMMIT OF HEADS OF STATE


……….………………....……………………

H.E. GENERAL SALVA KIIR MAYARDIT,

PRESIDENT, REPUBLIC OF SOUTH SUDAN



No comments :

Post a Comment