dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, June 29, 2016

PBZ YAADHIMISHA SHEREHE ZA MIAKA 50 KWA KUSAIDIA JAMII NA KUTEMBELEA HOSPITALI YA KIDONGOCHEKUNDU, ZANZIBAR!



Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akimkabidhi msaada wa magodoro 100 Kamishna Msaidizi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar Omar Salum Mgaza. hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Mafunzo Kilimani Zanzibar.

Baadhi ya magodoro 100 yaliotolewa msaada na PBZ kwa ajili ya matumishi ya Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar, ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar. hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Chuo cha Mafunzo Kilimani Zanzibar. 


Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ akizungumza na Maofisa wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar wakati wa kikabidhi msaada wa magodoro kwa ajili ya Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Mafunzo Kilimani Zanzibar.
Kamishna Msaidizi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar Omar Salum Mgaza akitowa shukrani kwa PBZ kwa msaada wao huo wa magodoro umeletwa wakati muafaka na kuwata taasisin nyengine kujitokeza kutoa misaada.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg.Juma Ameir akisalimiana na Muuguzi Dhamana wa Hospitali ya Kidongochekundu Zanzibar Ndg. Haji Vuai Hilal, wakati walipofika katika hospitali hiyo ya Mental kutowa misaada ya mashuka 200 kwa ajili ya hospitali hiyo. katikatika Afisa Masoko wa PBZ Ndg. Mohammed Nuhu. 
Afisa Masoko wa PBZ Ndg Mohammed Nuhu akisalimiana na Muuguzi Dhamana wa Hospitali ya Mental Kidongochekundu Zanzibar Haji Vuai Hilal. 
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Juma Ameir akizungumza na Uongozi wa Hospital ya Mental Kidongochekundu Zanzibar wakati wa kutembelea hospitali hiyo na kutoa msaada wa mashuka 200 ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya hospitali hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akikabodhi msaada wa mashuka kwa ajili ya hospitali ya Mental Kidogochekundu Zanzibar akipokea msaada huo Muuguzi Dhamani wa hospitali hiyo Ndg Haji Vuai Hilal. ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ kushaidia jamii Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akikabodhi msaada wa mashuka kwa ajili ya hospitali ya Mental Kidogochekundu Zanzibar akipokea msaada huo Muuguzi Dhamani wa hospitali hiyo Ndg Haji Vuai Hilal. ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ kushaidia jamii Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg. Juma Ameir akimkabidhi mmoja wa mgonjwa katika hospitali hiyo Bi Amina Mwinyi msaada wa tende kwa ajili yao katika kipindi hichi cha mfungo wa mwezi wa ramadhani.
Mmmoja wa mgonjwa katika hospitali Bi Amina Mwinyi, hiyo akitowa shukrani kwa niaba ya wezake kwa uongozi wa PBZ kwa msaada wao huo kwao na kuuthamini na kuwataka na Wananchi wengi kujitokeza kuwasaidia kwa vitu mbalimbali. 
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg. Juma Ameir akikabidhi msaada wa tenda mmoja wa wagonjwa wa hospitali hiyo Ndg. Mrisho Idrisa Hussein.

Muuguzi Dhamana wa Hospitali ya Mental Kidongochekundu Zanzibar Ndg Omar Vuai Hilal akitowa shukrani kwa Uongozi wa PBZ na Wafanyakazi wao kwa msaada wao huo katika hospitali hiyo.

Wafanyakazi wa PBZ wakijumuika na Mkurugenzi Mtenda wa PBZ Ndg Juma Ameir katika kutoa huduma kwa wateja ikiwa ni shamrashamra za kuadhimisha miaka 50 ya PBZ tangu kuazishwa kwa benki hiyo wakiwa katika Tawi la Malindi Zanzibar. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar Ndg Juma Ameir akitowa huduma kwa Wateja wa PBZ katika tawi la PBZ Malindi, Pbz imetimisha miaka 50 tangu kuazishwa kwa kwake Zanzibar. 
Wateja wa PBZ wakipita huduma za Kibenki katika Tawi la PBZ Malindi Zanzibar. 
Meneja wa Benki ya Watu wa Zanzibar Tawi la Malindi akitowa huduma kwa wateja wao akiwa na Afisi wa PBZ wakati wa shamrashamra za kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akitowa zawadi kwa Wateja wa PBZ ikiwa ni shamrashamra za kusherehekea miaka 50 ya PBZ kuazisha kutowa huduma za Kibenki Zanzibar.
Wateja wa PBZ wakiwa katika Tawi la Malindi Zanzibar wakisubiri kupata huduma za Kibenki katika tawi hilo. 
Wateja wakipatya huduma katika Benki hiyo Tawi la Malindi Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ akitowa zawadi kwa wateja wa PBZ Tawi la Malindi Zanzibar.
Mteja wa PBZ Zanzibar akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na huduma za Kibenki, wakati wa shamrashamra hizo za kusherehekea miaka 50 ya PBZ na kuwataka kuboresha zaidi huduma zao kwa wateja.

Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ akizungumza na waandishi wa habari malengo na changamoto za PBZ kwa wateja wake na malengo yao kutowa huduma kwa Wateja wao na kuboresha zaidi huduma zao. 
Afisa wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar Ndg Jaha akitowa huduma za kibenki kwa Wateja wao katika tawi hilo PBZ inatimiza miaka 50 tangu kuazishwa kwake. 
Afisa Manunuzi wa PBZ Bi Mwanaidi Ramadhani akitowa huduma za Kibenki kwa Wateja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar, Maofisa wa PBZ wameungana na wafanyakazi wa Matawi la PBZ kutowa Huduma za Kibenki kuadhimisha miaka 50 ya PBZ tangu kuazishwa kwake. 
Meneja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar akitowa huduma za Kibenki kwa Wateja wa PBZ ikiwa ni shamrashamra za kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar.
Meneja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar akizungumza na waandishi wa habari wakati wa shamrashamra za kutimia miaka 50 ya PBZ Zanzibar.
Afisa manunuzi wa PBZ Bi Mwanaidi Ramadhani akitoa zawadi kwa Wateja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar ikiwa ni kuadhimisha miaka 50 ya PBZ tangu kuazishwa kwake mwaka 1966-2016
Mteja wa PBZ akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na huduma za PBZ ni nzuri na kuwataka kuziboresha zaidi katika kipindi kijacho kwa wateja wao na kuwataka kuongeza huduma na ATM na kuziboresha zaidi huduma hizo kuwafikia hadi wananchi wa vijiji kupata huduma hii ya ATM huko mashamba.

Imetayarishwa na OthmanMapara. Zanzinews.com
email othmanmaulid@gmail.com

No comments :

Post a Comment