Streamed live on Aug 11, 2016
Rais Magufuli: Ndugu zangu uchaguzi umekwisha hakuna aliyeshida wala aliyeshindwa bali Watanzania wote tumeshinda.
Rais Magufuli: Niliahidi jiji la Mwanza litakuwa jiji la biashara tumeanza naomba mtuamini.
Rais Magufuli: Watumishi walikuwa wanachukua ndege wanaenda Dubai wanafanya siku 3 au 4 wanarudi kwa gaharama za watoto wa masikini.
Rais Magufuli: Mpaka sasa wafanyakazi hewa bado wapo na nitaendelea kutumbua.
Rais Magufuli: Tumeanza kutoa fedha bil 18.77 tulizoziokoa kwenye hao mafisadi tukazipeleka kwenye elimu watoto wasome bure.
Rais Magufuli: Wale Wabunge watiifu ambao hawakuziba midomo na kutoka nje, walipitisha tril. 29.5 za bajeti.
Rais Magufuli: Katika fedha hizo tunataka tununue ndege 3 kubwa, air Tanzania ilikuwa na kandege kamoja.
Rais Magufuli: Fedha ambazo tumetenga kwenye bajeti hii hazijawahi kutengwa toka dunia iumbwe.
Rais Magufuli: Tanzania tulikuwa tumezoea masherehe kweli, wakubwa serikalini wakiona kuna sherehe wanajipanga kula.
Rais Magufuli: Nimeambiwa kandarasi anatakiwa akabidhi hii kazi mwezi wa 12, unanisikia, nikisema nimesema.
Rais Magufuli: Wewe kandarasi ukichelewesha mradi, tena ninyi Wahehe mkichukia mnajinyonga, basi utajinyongea hapo hapo darajani.
Rais Magufuli: Upanuzi wa barabara ya Airport usiishie Pasiansi muongeze mpaka Airport na mimi hela nitawaletea.
Rais Magufuli: Tunataka tuanze kutengeneza nguo kisha tuvae, alafu mitumba tuwapelekee Ulaya.
Rais Magufuli: Wakakataa kuingia Bungeni, wakaziba midomo na plastiki, walisahau wangeziba na masikio, wakatoka na Bungeni.
Rais Magufuli: Hakuna ulazima wa mtu unavua samaki mpaka vifaranga, mlinichagua nami nitawaambia ukwe.
Rais Magufuili: kama kuna mtu alichoma makokoro ni mimi, na samaki waliongezeka.
Rais Magufuli: Wanapita kuna polisi, uhamiaji, TRA, lazima tulinde rasilimali yetu ili watanzania waweze kufaidika.
Rais Magufuli: Hizo zana zinapitishwa kwenye mipaka, shikeni na hilo gari mtaifishe moja kwa moja kwa sababu hayapiti angani.
Rais Magufuli: Waziri wa Ushirika, ni heri ukose kula, mimi nitakuchagua kwenye viti maalum, lakini mali za Nyaza zirudi.
Rais Magufuli: Nitoe agizo, ni lazima pawe na maeneo mbali mbali, muweze kufanya biashara, ila mkubaliane.
Hili blog ni kuhusu Tanzania na dunia nzima kwa ujumla. Pita kila siku kwa habari moto moto. (This blog is about Tanzania and the world as a whole. Pass-by everyday for breaking news). ***********************KARIBUNI NYOTE / YOU ARE ALL WELCOME!***********************
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments :
Post a Comment