dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, August 15, 2016

Mazishi ya Mzee Aboud Jumbe Mwinyi Zanzibar leo (picha)!

Viongozi wa kitaifa wakishiriki katika sala ya kumwombea Ras wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, marehemu Alhaj Abood Jumbe iliyofanyika kwenye msikiti, Mwembeshauri Zanzibar Agosti 15, 2016. Kutoka kushoto ni Makamu wa Rais, Mstaafu, Dkt. Mohammed Bilal, Rais Mstaafu wa Zanzibar, Aman Karume, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein.
Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, Alhaj Abood Jumbe katika mazishi yaliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Migombani Zanzibar Agosti 15, 2016.
Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohammed Shein, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Rais Mstaafu wa Zanzibar, Aman Karume, Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Ghalib Bilai wakiwa katika mazishi ya Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, Alhaj Abood Jumbe yaliyofanyika nyumbani kwa marehemu Migombani, Zanzibar Agosti 15, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka udongo kwenye kaburi la Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar Alhaj Abood Jumbe katika mazishi yaliyofanyika nyumbani kwa Marehemu Migombani Zanzibar, Agosti 15, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Ghalib Bilal baada ya mazishi ya Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, Alhaj Abood Jumbe yaliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Migombani Zanzibar Agosti 15, 2016.
 Jeneza lililobeba mwili wa Marehemu Aboud Jumbe likiwasili nyumbani kwa marehemu Migombani, Zanzibar
 Watoto, Ndugu, jamaa na Viongozi mbali mbali wakipokea mwili wa Marehemu Mzee Aboud Jumbe mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Migombani ,Zanzibar.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki dua maalum mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi ambaye alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  ,nyumbani kwa marehemu Migombani Zanzibar.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati)akishiriki dua maalum kwenye msiba wa Mzee Aboud Jumbe nyumbani kwa marehemu Migombani , Zanzibar wengine pichani ni Mke wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mama Mwanamema Shein (kushoto) kulia ni mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa.
Aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mmapinduzi ya Zanzibar ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha wananchi (CUF) MaalimSeif Shariff Hamad akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa walipohudhuria Mazishi ya aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Rais Mstaafu wa awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alhaji Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa walipohudhuria Mazishi ya aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Ally Mohamed Shein akimueleza jambo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa walipohudhuria Mazishi ya aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Baadhi ya Viongozi wa Serikali na Viongozi wastaafu wakifuatilia shughuli ya  Mazishi ya aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Mwili wa aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud ukishushwa kaburini.
Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Ally Mohamed Shein akiweka mchanga kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiweka mchanga kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William akiweka mchanga kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mohamed Gharib Bilali akiweka mchanga kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Edward Lowassa akiweka mchanga kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mmapinduzi ya Zanzibar ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha wananchi (CUF) MaalimSeif Shariff Hamad akiweka mchanga kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi akiweka mchanga kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza katika Mazishi wakiweka mchanga kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe leo Mjini Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe.Mohamed Aboud Mohamed akisoma wasifu wa Marehemu Mzee Aboud Jumbe wakati wa Mzishi yaliyofanyika Nyumbani kwake Mjini Zanzibar.
Sheikh akisoma Duaa Mara baada ya kuuhifadhi Mwili wa Mzee Aboud Jumbe
Mtoto Mkubwa wa Marehemu Bw. Mustafa Aboud Jumbe akitoa shukrani kwa viongozi wa serikali na wananchi waliojitokeza katika kumuaga Mzee Aboud Jumbe na kuishukuru serikali kukubali kuiruhusu familia kufanya taratibu za mazishi kama alivyoelekeza Marehemu Mzee Aboud Jumbe wakati wa uhai wake. 
Picha na Hassan Silayo

No comments :

Post a Comment