dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, September 8, 2016

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi watembelea miradi mbalimbali ya Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Pemba!

AFISA wa Mamlaka ya Maji (ZAWA) Wilaya ya Micheweni Ali Rajab Khatib, akitoa maelezo ya mradi wa maji uliojengwa na TASAF II katika shehia ya Wingwi Njuguni, kwa wajumbe wa kamati ya Baraza la Wawakilishi ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu Kitaifa, wakati walipotembelea miradi mbali mbali iliyo chini ya Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Ofisi ya Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

WAJUMBE wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa Kitaifa, wakipata maelekezo ya mashine ya maji iliyotolewa na kuwekwa nyengine ambayo kwa sasa haikidhi mahitaji ya wananchi katika kisima hicho, kilicho jengwa na mradi wa TASAF II katika shehia ya Wingwi Njugumi Wilaya ya Micheweni Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

MWENYEKITI wa Kamati ya Baraza la wawakilishi ya kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa kitaifa, Mwakilishi wa jimbo la Konde Mhe:Omar Said Abeid, akizungumza afisa wa Mamlaka ya Maji ZAWA Wilaya ya Michweni Ali Rajab Khatib, wakati kamati yake ilipotembelea mradi huo wa maji huko Wingwi Njuguni.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

MJUMBE wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa Kitaifa, Mwakilishi wa Jimbo la Mpendae, Mhe:Mohamed Said Dimwa, akieleza jambo wakati wajumbe wa kamati hiyo walipokagua mradi wa maji safi na salama Wingwi Njuguni.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
MJUMBE wa kamati ya Baraza la Wawakilishi ya kusimamia Ofisi za Viongozi wa kuu wa Kitaifa, Mwakilishi wa jimbo la Tunguu Mhe:Simai Mohamned Simai (Mpaka Basi), akitoa mawazo juu ya mradi wa maji safi salama Wingwi Njuguni uweze kufikia malengo.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

AFISA mdhamini Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Pemba, Mhe:Ali Salum Mata, akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa kamati wa baraza la wawakilishi, juu ya Mradi wa Maji safi na salama Wingwi Junguni.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

WAJUMBE wa kamati ya baraza la Wawakilishi ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wa kuu wa Kitaifa, Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe:Simai Mohamed Simai na Mwakilishi wa Jimbo la Mpendae Mhe:Mohamed Said Dimwa wakisokota kamba kwa kutumia mashine maalumu, huku wajumbe wenzao wakiwaangalia juu ya ufanyaji wa kazi hiyo.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)


NDEGE kubwa aina ya Precision Air, ikiwa inashusha mizigo baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa Karume Air Port Kisiwani Pemba, kama inavyoonekana katika Picha .(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

MWAKILISHI wa Jimbo la Mpendae Mhe:Mohamed Said Dimwa, akiwauliza maswali wafanyakazi waliopo katika mashine ya kuchunguzia Mizigo katika Uwanja wa Ndege wa Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

WAJUMBE wa kamati ya Baraza la Wawakilishi ya kusamamia ofisi za Viongozi wa kuu wa Kitaifa, wakiwa katika kikao cha pamoja cha Tathmini ya ziara yao, kilichofanyika Ofisi ya Makamu wa Pili Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais Zanzibar Mhe:Mohamed Aboud Mohamed, akizungumza wajumbe wa kamati ya baraza la wawakilishi ya kusimamia Ofisi ya Viongozi wa kuu wa Kitaifa, huko katika ukumbi wa Tasaf Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

No comments :

Post a Comment