dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, October 29, 2016

Faida 48 za Juisi ya Tangawizi ambazo ulikuwa huzijuwi bado!

Huwa inanishangaza sana ninapoutafakari ukuu wa Mungu kwa namna ambayo ametupa mimea mbalimbali mhimu kwa ajili ya afya zetu – Mwanzo 1:29. Maelezo yafuatayo kuhusu tangawizi yatakupa wewe ujuzi wa mmea mwingine wa asili usio na madhara ya kikemikali na kusaidia mwili wako kuwa na afya nzuri na ya kupendeza.

Tafiti mpya zinazidi kuonyesha namna mmea huu ulivyo wa mhimu kwa afya ya binadamu ikihusisha uwezo wake wa kudili na aina mbalimbali za kansa mwilini na tafiti nyingine zinaendelea kufanyika.

Tangawizi inaweza kuwekwa karibu kwenye kila chakula, iwe ni katika kuilainisha nyama nyekundu, kuongeza radha katika nyama au samaki, kama chai, kwenye juisi na kadharika. Binafsi napenda ikiwa kwenye juisi ya matunda ndiyo inakuwa tamu zaidi na inaenda kufanya kazi mwilini haraka zaidi.Tangawizi ni zao la kibiashara na ni rahisi kutoka kimaisha kama utaamua kulima tangawizi ingawa ni zao la miezi mingi lakini ukivumilia utakula bata tu, gunia moja linauzwa kati ya laki 3 hadi 6 wakati wa msimu mzuri.

Tangawizi iliorodheshwa kwa mara ya kwanza na serikali ya Marekani kama dawa kwa ajili ya binadamu kati ya mwaka 1820 na 1873.

Tangawizi huongezwa pia katika vinywaji vingi vya viwandani zikiwemo soda ili kupata radha nzuri zaidi.

Leo nimekuletea hii juisi ya tangawizi, nimetumia tangawizi mbichi za ukubwa wa kati nne, parachichi moja na asali mbichi vijiko vikubwa saba na na maji lita moja na nusu.

Kazi 48 za tangawizi mwilini

  1. Huondoa sumu mwilini haraka sana
  2. Huua bakteria wa aina nyingi mwilini hata salmonella ndani ya mwili hata juu ya ngozi
  3. Kuna viua vijasumu (antibiotics) vya asili viwili kwenye tangawizi
  4. Huondoa uvimbe mwilini
  5. Huondoa msongamano mapafuni
  6. Tangawizi inayo ‘zingibain’ ambayo huua vimelea mbalimbali vya magonjwa na mayai yake
  7. Huondoa maumivu ya koo
  8. Huua virusi wa homa
  9. Huondoa maumivu mbalimbali mwilini
  10. Huondoa homa hata homa ya baridi (chills)
  11. Hutibu saratani ya tezi dume. Tangawizi huua kimeng’enya ambacho ni chakula cha seli za kansa ya tezi dume kiitwacho ‘5-LO enzymes’ na seli hizo za kansa hufa ndani ya masaa mawili au manne bila hicho kimeng’enya.
  12. Tangawizi ina kiinilishe mhimu sana ambacho huzuia kuongezeka kwa seli za kansa ya kongosho kiitwacho kwa kitaalamu kama ‘gingerol”
  13. Hutibu kansa zinazoweza kusababishwa na kupata choo kigumu muda mrefu (constipation-related cancer)
  14. Ni dawa nzuri kwa kansa ya kwenye damu (leukemia)
  15. Ni dawa nzuri dhidi ya kansa ya mapafu (lung cancer)
  16. Huzuia kujizalisha kwa bakteria aitwaye ‘Helicobacter pylori’, bakteria huyu ndiye husababisha vidonda vya tumbo mwilini, pia hutibu kiungulia, na kanza mbalimbali za tumbo
  17. Ni msaada sana katika kuzuia na kutibu kansa ya titi
  18. Hutibu kanza za kwenye kizazi na kanza za kwenye mirija ya uzazi
  19. Huongeza msukumo wa damu
  20. Husaidia kuzuia shambulio la moyo
  21. Huzuia damu kuganda
  22. Hushusha kolesto
  23. Husafisha damu
  24. Husaidia watu wenye kukakamaa kwa mishipa
  25. Hutibu shinikizo la juu la damu
  26. Husafisha utumbo mpana
  27. Hupunguza mishtuko kwenye utumbo mpana na tumbo kuunguruma
  28. Huondoa GESI TUMBONI KIRAHISI ZAIDI
  29. Husaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula
  30. Dawa nzuri ya kuondoa uchovu
  31. Husaidia kuzuia kutapika. Husaidia hata wale wanaosafiri baharini wasipatwe na kichefuchefu
  32. Husaidia kuondoa maumivu kutokana na mkao mmoja wa mrefu ama kusimama au kukaa
  33. Husaidia uzalishwaji wa juisi vimeng’enya kwa ajili ya kumeng’enya chakula
  34. Husaidia kuzuia kuharisha
  35. Husaidia mfumo wa upumuaji na kutuliza dalili za pumu
  36. Hutibu tatizo la miguu kuwaka moto
  37. Hutibu homa ya kichwa
  38. Hutibu maumivu ya tumbo wakati wa hedhi
  39. Hutibu homa za asubuhi hata kwa mama mjamzito
  40. Husaidia kupunguza homa ya baridi yabisi (helps reduce inflammation of arthritis)
  41. Huimarisha afya ya figo
  42. Husaidia kupunguza uchovu unaotokana na matibabu yaliyopita ya mionzi
  43. Ina madini ya potassium ya kutosha
  44. Ina madini ya manganese ambayo ni mhimu katika kuuongeza mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali.
  45. Ina kitu kinaitwa ‘silicon’ ambacho chenyewe kazi yake hasa ni kuongeza afya ya ngozi, nywele, meno na kucha
  46. Husaidia umeng’enywaji wa madini ya calcium
  47. Pia ina vitamini A, C, E, B-complex, chuma, zinki , magnesium, phosphorus, sodium, calcium, na beta-carotene
  48. Hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita

No comments :

Post a Comment