dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, October 12, 2016

Mwenyekiti wa AFP azungumza na waandishi wa habari!

 Waziri asiekuwa na Wizara Maalum na Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima AFP Said Soud Said akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na kuwataka Wazanzibari kuwekeza ili kujikwamua kiuchumi,katika ukumbi wa Jumba la Utamaduni Rahaleo Zanzibar.
 Waziri asiekuwa na Wizara Maalum na Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima AFPSaid Soud Said akifafanua jambo alipofanya mazungumzo na Waandishi wa Habari kuhusiana na kuwataka Wazanzibari kuwekeza ili kujikwamua kiuchumi,katika ukumbi wa Jumba la Utamaduni Rahaleo Zanzibar.kulia ni Mkuu wa Habari  Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Ramadhani Ali.

 Baadhi ya Waandishi wa Habari waliohudhuria katika Mkutano wa Waziri asiekuwa na Wizara Maalum na Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima AFP Said Soud Said  alipofanya mazungumzo nao kuhusiana na kuwataka Wazanzibari kuwekeza ili kujikwamua kiuchumi,katika ukumbi wa Jumba la Utamaduni Rahaleo Zanzibar.
 Muandishi wa Habari kutoka Hits FM Jazaa Kombo akiuliza maswali katika Mkutano wa Waziri asiekuwa na Wizara Maalum na Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima AFP Said Soud Said  kuhusiana na kuwataka Wazanzibari kuwekeza ili kujikwamua kiuchumi,katika ukumbi wa Jumba la Utamaduni Rahaleo Zanzibar.

Muandishi wa Star Tv Abdalla Pandu akiuliza maswali katika  Mkutano wa Waziri asiekuwa na Wizara Maalum na Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima AFP Said Soud Said  kuhusiana na kuwataka Wazanzibari kuwekeza ili kujikwamua kiuchumi,katika ukumbi wa Jumba la Utamaduni Rahaleo Zanzibar.

PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

Na Mwanaisha Mohammed-Maelezo                              

Wazanzibari wametakiwa kujikusanya na kuanzisha  makampuni makubwa  ya  kuwekeza  badala ya kusubiri wawekezaji kutoka nje ili kusaidia jamii na kuharakisha maendeleo.

Akizungumza na waandishi wa Habari katika studio ya zamani ya utangazaji Rahale, Mwenyekiyi wa Chama Cha Wakulima (AFP) Said Soud  amesema wazanzibari wanayo nafasi nzuri ya kuwekeza hasa katika sekta ya uvuvi wa bahari kuu, kilimo na ufugaji pamoja na michezo.

Saidi Soud  ambae pia ni Waziri asiekuwa na Wizara maalum katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar amesema iwapo wananchi watajikusanya na kutafuta wafadhili kwa ajili ya kuwekeza wataweza kuisaidia nchi kwa kuwapatia vijana ajira badala ya vijana wengi kusubiri ajira za serikali baada ya kumaliza masomo.

“Wawekezaji wazalendo wananafasi kubwa katika kuhudumia jamii bila kusubiri wawekezaji kutoka nje kuwekeza vitega uchumi vyao, ”alisisitiza Mwenyekiti wa chama cha AFP.

Alisema ni jambo zuri kuwakaribisha wawekezaji kutoka nje kwa vile wanakuja na teknolojia ya kisasa lakini jambo zuri watakapofika  wakute wazalendo wenyewe wanaendelea kuwekeza.

Amewashauri  wananchi kuwa wabunifu na  kuachana na  uvvivu wa kufikiri ili kupiga hatua ya haraka kuleta maendeleo.

“Wazanzibar acheni  dhana ya kufikirishwa  kuna fursa nyingi za kuwekeza ambazo zitapelekea kujikwamua na umasikini,”alisema Said Soud.

 Aliishauri jamii  kujituma na kutumia rasilimali  na fursa nyingi zilizopo  huku Serikali ikiendelea kuweka mazingira mazuri ya wananachi  kuendeleza  shughuli zao za maisha  na kupunguza umasikini.

Akizungumzia hali ya kisiasa Zanzibar, amesema ni nzuri na amewataka wananchi kuvipuuza  vikundi na wanasiasa wanaozungumzia kufanyika uchaguzi mwengine kabla ya mwaka 2020.

Amewataka wananchi kuelekeza nguvu zao katika kufanyakazi badala ya kusikiliza maneno ambayo hayana tija kwao na hayasaidii kuharakisha maendeleo yao.
                                                       
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.

No comments :

Post a Comment