dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, November 10, 2016

Rasi Dk Shein awaapisha Naibu Mawaziri ikulu leo!

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ  Mhe,Shamata Shaame Khamis akiikariri hati ya kiapo kabla ya kuapishwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Unguja,(kulia)Naibu Waziri wa Kazi,Uwezeshaji,Wazee,Wanawakena Watoto Mhe,Shadia Mohamed Suleiman,[Picha na Ikulu.]10/11/2016.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mhe,Mihayo Juma Nhunga,akiikariri hati ya kiapo kabla ya kuapishwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Unguja,(kushoto)Naibu Waziri wa Kazi,Uwezeshaji,Wazee,Wanawake na Watoto Mhe,Shadia Mohamed Suleiman,[Picha na Ikulu.]10/11/2016.


 Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mhe,Saidi Hassan Said (kulia) akiwa na Washauri wa Rais wa Zanzibar ni miongoni mwa Viongozi waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Manaibu Mawaziri wa Wizara mbali mbali za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar leo Ikulu Mjini Zanzibar, [Picha na Ikulu.] 10/11/2016.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  akimuapisha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mhe,Mihayo Juma Nhunga, katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 10/11/2016.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  akimuapisha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ  Mhe,Shamata Shaame Khamis katika  hafla iliyofanyika leo Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 10/11/2016
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  akimuapisha Naibu Waziri wa Kazi,Uwezeshaji,Wazee,Wanawake na Watoto Mhe,Shadia Mohamed Suleiman, katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 10/11/2016.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati)  akiwa na Viongozi mbali mbali baada ya kuwaapisha Naibu Mawaziri katika Wizara mbali mbali hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa  Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 10/11/2016.

  
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
 Zanzibar                                 10.11.2016
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha Manaibu Waziri wapya ambao aliwateuwa hivi karibuni kushika nyadhifa katika Wizara mbali mbali za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Walioapishwa ni Mihayo Juma Nhunga kuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Shamata Shaame Khamis, Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ na Shadya Mohamed Suleiman, kuwa Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto.

Hafla ya kuwaapisha viongozi hao ilifanyika Ikulu Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Miongoni mwa viongozi hao ni Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Gavu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mohammed Aboud, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Haji Omar Kheri.  

Wengine ni  Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Maudline Castico,Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Mkuu wa  Mkoa wa Mjini Magharibi  Ayoub Mohammed Mahmoud, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib, Washauri wa Rais wa Zanzibar, Wakuu wa Vikosi vya SMZ na viongozi wengine wa Serikali. 

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822  
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments :

Post a Comment