Na Muhammed Khamis
Jamii Nchini imeombwa kujitolea kusaidia kwa hali na mali kiasi chochote kile walichonacho kwa ajili ya kusidia faimilia ya Bwana Salim Nassor wa Mwanakwerekwe mjini Unguja kufuatia maafa ya moto yalioteketeza nyumba yake juzi kwa moto kupitia hitilafu ya umeme.
Akizungumza na Mazrui Media mzee mwenye nyumba hio amesema tukio hilo la kuunguliwa na nyumba yake limepoteza kila kitu kwenye nyumba hio kiasi ambacho yeye na familia yake wamekosa hata nguo ya kuvaa kwa sasa.
‘’Hizi nguo unazoziona nimevaa hapa nimepewa na majirani zangu sikubakishwa hata na nguo moja mimi na familia yangu’’alieleza kwa masikitiko mzee huyo huki akitokwa na machozi.
Alisema anaamini yote ni mipango ya Mungu lakini ana imani kubwa wananchi mbali mbali wenye uwezo wanaweza kumsaidia kwa hali yoyote ile yeye na familia yake.
Aidha aliwatabahisha wale wote wenye uwezo kujitolea kumsaidia na hakika msaada wao wataukuta siku moja mbele ya Mwenyezimungu na wanaweza kuwasiliana nae moja kwa moja kupitia namba hii 0777485690.
No comments :
Post a Comment