dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, November 26, 2016

UWEKEZAJI WA TANESCO WAFIKIA SHILINGI TRILIONI 5.35, NI MKUBWA KATIKA HISTORIA YA UMEME NCHINI!

 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini, (TANESCO), Mhandisi Felchesmi Mramba, (katikati), akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo Novemba 24, 2016. Alikuwa akitoa ufafanuazi kuhusu masuala muhimu ya TANESCO. Wengine pichani, kulia ni Meneja wa Vyuo vya TANESCO, Mhandisi Said Msemo na kushoto ni Kaimu Meneja Uhisano wa Shirika hilo, Leila Muhaji.
 Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo
  Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo
 Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji, (kushoto), akizunguzma jambo

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
SERIKALI kupitia Shirika lake la umeme nchini TANESCO limefanya uwekezaji mkubwa kwenye miradi mbalimbali ya umeme yenye thamani ya Shilingi Trilioni 5.35, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Mhandisi Felchesmi Mramba amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo Novemba 24, 2016.

Akitoa ufafanuzi juu ya masuala mbalimbali muhimu ya Shirika hilo, Mhandisi Mramba alisema, “Katika historia ya sekta ya umeme, haijawahi kutokea uwekezaji mkubwa kufanyika kwa wakati mmoja kama ilivyo sasa, Miradi yote ya umeme inayoendelea na ambayo tayari iemtengewa fedha ina thamani ya Shilingi Trilioni 3.85, na majadiliano kati ya Serikali na Exim Bank ya mradi wa Dar es Salaam-Arusha wa Shilingi Trilioni 1.5 yakiwa katika hatua za mwisho.” Alifafanua Mhandisi Mramba.
“ Uwekezaji huu unathibitisha kwamba nia ya Serikali ya awamau ya tano ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda sio ya maneno matupu bali inaambatana na vitendo kwa uwekezaji madhubuti kwenye umeme.” Alisema.

Mhandisi Mramba alitaja Miradi hiyo mikubwa ya umeme kuwa ni pamoja na ule wa upanuzi wa Kinyerezi I, Kinyerezi II, mradi wa Backbone, Kenya-Tanzania, TEDAP, Makambako-Songea, Uboreshaji umeme jijini Dar es Salaam, City Centre-Dar es Salaam, Electricity V, Bulyanhulu-Geita, Geita Nyakanazi na Rusumo Power Plant (T), miradi yote hii ikiwa na jumla ya thamani ya Shilingi Trilioni 3.85.

Akifafanua zaidi kuhusu uwekezji huo, Mhandisi Mramba alisema, Miradi yote ambayo thamani yake imetajwa haihusishi Miradi ya usambazaji umeme Vijijini chini ya mpango wa REA.
Akizungumzia utaratibu mpya wa manunuzi,(Procumbent), Mhandisi Mramba alisema, TANESCO imechukua hatua kadhaa ili kuboresha manunuzi ambapo kuanzia sasa makampuni yanayomilikiwa na mtu mmoja kuhodhi manunuzi ya Shirika hilo, na kwamba zabuni zote zilizotangazwa kuanzia mwaka huu wa fedha, haitaruhusiwa kampuni moja kuwa na mikataba miwili kwa wakati mmoja.
Akifafanua zaidi alisema, Katika zabuni moja haitaruhusiwa kampuni moja kupewa zaidi ya Lot 1, “Hii imeanza kusaidia kuondoa ukiritimba katika manunuzi na kuwapa Watanzania wengi zaidi nafasi pana ya kushiriki katika zabuni za kusambaza vifaa vya umeme.” Alifafanua Mhandisi Mramba.

Aidha Mhandisi Mramba alisema, ili kuwezesha Watanzania wengi kushiriki katika uchumi wa nchi, TANESCO itanunua vifaa vya umeme vinavyozalishwa hapa nchini na kuachana na mtindo wa kuagiza kutoka nje.

“Mfano kwa nguzo za umeme tumewapa Sao Hill, ambao watatuuzia nguzo 96,500, na new Forest watatuuzia nguzo za umeme 9,668, na kwa upande wa Transfoma za umeme, kandarasi hiyo imepewa kampuni ya TANELEC itakayotuuzia transfoma 1,500” Alifafanua
Akieleza zaidi kuhusu ununuzi wa vifaa, Mhandisi Mramba alisema, kampuni ya East Africa Cables, intarajiwa kupewa kazi ya kusambaza waya na kuongeza kuwa utaratibu huo pia utatumika kwenye huduma nyingine kama vile Bima, ambapo alisema Shirika linatarajia kulitumia Shirika la Bima la Taifa, (NIC), kutoa huduma hiyo.

Akizungumzia kuhusu hali ya umeme, Mhandisi Mramba aliwahakikishia Watanzania kuwa kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Shirika hilo katika kuboresha miundombinu ya umeme, hakutakuwa na mgao wa umeme nchini na ndio maana kwa muda mrefu sasa hakuna mgao wa umeme.“Mwaka 2015 nchi ilikuwa na mgao wa umeme wa jumla ya MW300, na maeneo mengine yalikuwa na hali mbaya hususan Mwanza, Arusha na Kilimanjarolakini kwa sasa hali ya umeme katika mikoa yote na mingine ni nzuri hakuna mgao na kama ikitokea umeme umekatika ni matatizo ya kiufundi katika eneo dogo na kwa muda mfupi.” Alisema.

Hata hivyo alisema Shirika lake linaongeza juhudi za kusambaza umeme kwa watanzania wengi zaidi kote nchini, kutokana na uwekezaji wa miundombinu unaoendela kila kona ya nchi.
Mhandisi Mramba aliwaondoa wasiwasi wananchi kuhusu ombi la Shirika hilo la kuongeza asilimia 18.9 ya bei ya umeme kuanzia Januari mwakani, kwa kusema ongezeko hilo halitaathiri watumiji wa kawaida majumbani. “Tunachoomba kutoka kwa Msimamizi (Regulator), ni kufanya mabadiliko ya kutenganisha watumiaji umeme wa majumbani na wale wanaotumia kibiashara kama vile mabango ya matangazo, kwani hivi sasa wote wanalipa gharama sawa na hili si sawa.” Alisema.

Aliwaasa wananchi kuridhia ongezeko hilo kwani Shirika limo katika jitihada kubwa za kuhakikisha Wananchi wengi zaidi wanapatiwa umeme kwa kufikisha miundombinu ya umeme kwenye maeneo mbalimbali ya nchi, ambapo gharama za kufanya hivyo zimeongezeka.

No comments :

Post a Comment