dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, December 6, 2016

Mzozo wazuka upya kuhusu mpaka wa Tanzania na Malawi!


  • Ramani ya Tanzania inaonyesha kuwa eneo la Kaskazini Mashariki mwa ziwa hilo ni sehemu ya himaya yake.
Ramani mpya iliyotolewa na Tanzania ambayo inaonyesha kuwa inaamiliki nusu ya Ziwa linalozozaniwa la Malawi au Nyasa, imezua mzozo mpya na Malawi ambayo inasema kuwa ramani hiyo sahihi.

Ramani ya Tanzania inaonyesha kuwa eneo la Kaskazini Mashariki mwa ziwa hilo ni sehemu ya himaya yake, lakini Malawi nayo inadai kuwa eneo hilo lote ni lake.

Malawi imeomba Umoja wa Mataifa, Mungano wa Afrika na mashirika mengine ya kimataifa kuingilia kati.


Msemaji wa wizara ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Malawi, Rejoice Shumba amesema kuwa Malawi imeandika barua kwa mashirika makuu duniani ikiyataka kupuuzilia mbali ramani ya Tanzania.

Hii si mara ya kwanza Malawi imepinga ramani hiyo ya Tanzania.Msukosuko uliibuka mwaka 2011 wakati Malawi ilianza shughuli za kutafuta mafuta kwenye ziwa hilo.

Serikali ya Tanzania bado haijatamka lolote kukuhusu suala hilo.

Nini hasa kinazozaniwa?
Fahari ya nchi na maswala ya kujiendeleza kiuchumi kwa Malawi na Tanzania kila mmoja akisimama kidete kusisitiza msimamo wake.

Kwa Tanzania, ziwa hilo linajulikana kama Nyasa, wakati nchini Msumbiji inajulikana kama Lago Niassa.

Malawi na Tanzania ni koloni za zamani za Uingereza wakati Msumbiji ilikuwa chini ya ukoloni wa Ureno. Uingereza iliichukua Tanzania kutoka kwa Wajerumani baada ya wao kushindwa katika vita vya kwanza vya dunia.

Kando na ripoti za kuwepo mafuta na gesi katika ziwa hilo, ziwa lenyewe ni kivutio kikubwa cha watalii.

Malawi inasema inashauriana na Msumbiji kuhusiana na uchimbaji wa mafuta katika siku za baadaye ili kuzuia mzozo wa kidiplomasia .

Je hii ni mara ya kwanza kwa mzozo huu wa ziwa Malawi kutokea?
Hapana. Mapema miaka ya sitini, Malawi ilidai umiliki wa ziwa hilo kwa kuambatana na makubaliano ya mwaka 1890 Heligoland kati ya Uingereza na Ujerumani ambayo yalisema kuwa mpaka kati ya nchi hizo uko upande wa Tanzania.

Makubaliano hayo yaliafikiwa na Muungano wa Afrika na Tanzania ikaitikia ingawa shingo upande. Mzozo mpya kati ya nchi hizo ukaripotiwa tena kati ya mwaka 1967 na 1968.

Ulichipuka tena mwaka mwaka 2011, Malawi ilipotoa leseni ya kuchimba mafuta kwa kampuni ya British Surestream Petroleum Limited. Sehemu iliyotolewa kwa uchimbaji wa mafuta ni sehemu yenye mraba wa kilomita 20,000 sehemu ambayo Tanzania inasema ni yake.

Vyombo va habari viliripoti mwezi Julai mwaka 2012 kuwa mitumbwi ya wavuvi na ya watalii kutoka Malawi ilivuka na kuingia upande wa Tanzania

Tanzania nayo ikasema kuwa ingetafuta ushauri kutoka jamii ya kimataifa ikiwa nchi hizo hazingeweza kusuluhisha mzozo huo zenyewe.

Hofu ya hatua za kijeshi
Hofu ya mzozo kutokota na kuwa mbaya zaidi ilijitokeza mwaka 2012 wakati Tanzania iliposema kuwa ingelinda mipaka yake na kuzingatia sheria za kimataifa.

No comments :

Post a Comment