zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, June 18, 2017

POLE SANA MZEE YUSUF!



Mke wa mzee Yusuf, Marehemu Chiku Hamisi, hatimaye amezikwa kwenye Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam, shughuli ambayo imehudhuriwa na mamia ya waombolezaji.
Chiku alifariki Jumamosi jioni katika Hospitali ya Amana wakati akijifungua ambapo kichanga kilichokuwa tumboni mwake nacho kilifariki.
Chiku alipoteza maisha akisaidiwa na wauguzi kujifungua kwa njia ya upasuaji ambapo mwanaye aliyekuwa tumboni alifariki pia.
Shughuli za msiba na mazishi zilianzia nyumbani hapo Kariakoo Mtaa wa Amani na Livingstone ambapo mwili ulitolewa nyumbani hapo na kwenda kuswaliwa kwenye msikiti wa Manyema.
Baada ya sala mwili ulipelekwa makaburi ya Kisutu jijini hapa. 
Katika mazishi hayo Mzee Yusuf aliishiwa nguvu ambapo aliondolewa makaburini hapo kwa msaada wa waombolezaji.
Mzee Yusuf alikuwa Mkurugenzi wa Bendi ya Jahazi Modern taarab kabla ya baadaye kuamua kuachana na muziki wa kidunia na kumgeukia Mungu wake.

No comments :

Post a Comment