Hili blog ni kuhusu Tanzania na dunia nzima kwa ujumla. Pita kila siku kwa habari moto moto. (This blog is about Tanzania and the world as a whole. Pass-by everyday for breaking news). ***********************KARIBUNI NYOTE / YOU ARE ALL WELCOME!***********************
Sunday, June 18, 2017
POLE SANA MZEE YUSUF!
Mke wa mzee Yusuf, Marehemu Chiku Hamisi, hatimaye amezikwa kwenye Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam, shughuli ambayo imehudhuriwa na mamia ya waombolezaji.
Chiku alifariki Jumamosi jioni katika Hospitali ya Amana wakati akijifungua ambapo kichanga kilichokuwa tumboni mwake nacho kilifariki.
Chiku alipoteza maisha akisaidiwa na wauguzi kujifungua kwa njia ya upasuaji ambapo mwanaye aliyekuwa tumboni alifariki pia.
Shughuli za msiba na mazishi zilianzia nyumbani hapo Kariakoo Mtaa wa Amani na Livingstone ambapo mwili ulitolewa nyumbani hapo na kwenda kuswaliwa kwenye msikiti wa Manyema.
Baada ya sala mwili ulipelekwa makaburi ya Kisutu jijini hapa.
Katika mazishi hayo Mzee Yusuf aliishiwa nguvu ambapo aliondolewa makaburini hapo kwa msaada wa waombolezaji.
Mzee Yusuf alikuwa Mkurugenzi wa Bendi ya Jahazi Modern taarab kabla ya baadaye kuamua kuachana na muziki wa kidunia na kumgeukia Mungu wake.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments :
Post a Comment