Maelfu ya raia wa Zimbabwe jana walijitokeza barabarani hasa mjini Harare wakijiandaa kwa mkutano mkubwa unaoungwa mkono na chama tawala ZANU-PF katika jitihada za kuongeza shinikizo la kumtaka rais Mugabe ajiuzuulu,wakishikilia mabango yaliyoandikwa Mugabe Must Go.
Zanu-PF ndio chama kilichomsaidia Mugabe kuwa madarakani nchini kwa takriban miaka 40.
Kikubwa kinachozozaniwa ni nani atakayemrithi rais Mugabe atakapoochia madaraka.
Mugabe angependelea mkewe kumrithi lakini wapiganiaji wa uhuru nchini humo wanamtaka aliyekuwa makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa ambaye Mugabe alimfuta kazi wiki iliyopita, kutokana na uhasama mkubwa baina yake na mkewe rais Mugabe uliotokana na upiganiaji huo wa madaraka.
Zaidi ya hayo Bw. Mugabe angependa kuendelea kuwa uongozini hadi chama kitakapofanya mkutano wao mkuu mwezi ujao.
Wananchi wa Zimbabwe waliojawa na furaha wameandamana katika Jiji la Harare wakishinikiza rais Robert Mugabe ajiuzulu.
Waandamanaji hao wameonekana wakiwakumbatia wanajeshi kuwapongeza kwa uamuzi wa kuchukuwa udhibiti wa nchi hiyo tangu jumatano.
Maandamano hayo yanaungwa mkono na wanajeshi na wanachama wa chama tawala wa Zanu-PF, huku maveterani wa vita nao wakimtaka Mugabe aachie madaraka.
Waandamanaji wakiwa na picha za Mkuu wa Majeshi Jenerali Constatino Chiwenga pamoja na Makamu wa Rais Emerson Mnangagwa katika kuwapongeza








No comments :
Post a Comment