dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, November 15, 2017

Ziara ya Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Kutembelea Idara za Uhamiaji Unguja leo!



Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu (katikati), Akitoa Ushauri kwa Maofisa Waandamizi juu ya umuhimu wa Utanuzi wa Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharib Unguja, ili kukidhi ongezeko la wananchi wanaofika kupata huduma mbali mbali za Uhamiaji Mkoani humo. Aliyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kikazi Mkoani humo, Leo tarehe 15 Novemba, 2017. 
Mrakibu wa Uhamiaji, Gharib Saleh Suleiman (Kushoto), akitoa maelezo kwa Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu (Kulia), kuhusu Utoaji wa Vibali vya Ukaazi katika Kituo cha Uhamiaji, kilichoko ndani ya Mamlaka ya kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) wakati wa ziara ya kikazi iliyofanyika jana tarehe 14 Novemba, 2017. Kati kati ni Mfawidhi wa Kituo cha Uhamiaji –ZIPA, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji, Juma Sefu Juma.
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, Akisisitiza jambo wakati akiongea na Wafanyakazi wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharib Unguja (hawapo pichani), wakati alipofanya ziara ya kikazi Mkoani hapo, Leo tarehe 15 Novemba, 2017. Kulia ni Kaimu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharib, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Othman Khamis Salum.
Afisa Uhamiaji Wilaya ya Magharib “B” Kamishna Mwandamizi wa Uhamiaji, Longido L. Katovi, akitoa ufafanuzi kwa Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, kuhusu uendeshaji wa Doria na Misako zinavyosaidia Udhibiti wa Wahamiaji Haramu katika Wilaya zilizomo ndani ya Mkoa wa Mjini Magharib Unguja, wakati wa ziara ya kikazi Mkoani humo, Leo tarehe 15 Novemba, 2017. 
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, Akitoa Nasaha kwa Watumishi wa Idara ya Uhamaiji, Mkoa wa Mjini Magharib Unguja, kufanyakazi kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu za kazi, Nidhamu, Weledi, Uwajibikaji na Utaoji wa Huduma unaozingatia Maadili ya Kazi. Aliyasema hayo Leo tarehe 15 Novemba, 2017 wakati alipofanya ziara ya kikazi Mkoani humo. Kulia ni Kaimu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharib, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Othman Khamis Salum na Kushoto ni Afisa Utumishi Mkuu wa Uhamiaji Zanzibar, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Abullah Mbarouk Ramsa.
Mkaguzi wa Uhamiaji Malik Mohamed Abdallah akichangia hoja zilizojadiliwa katika kikao cha pamoja cha Wafanyakazi wa Mkoa wa Mjini Magharib Unguja na Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, wakati alipofanya ziara ya kikazi Mkoani humo, Leo tarehe 15 Novemba, 2017.
Wateja waliofika kupata huduma za Uhamiaji katika Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharib Unguja, wakifurahia kauli iliyotolewa na Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, kwamba Idara yake imejipanga kutoa Huduma bora kama zilizivyoainishwa kwenye Mkataba wa Huduma kwa Wateja. Aliyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kikazi Mkoani humo, Leo tarehe 15 Novemba, 2017.

No comments :

Post a Comment