Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akizungumza na Balozi mpya wa China nchini, Wang Ke, wakati balozi huyo alipomtembelea Masauni ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, kwa lengo la kujadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya China na Tanzania. Katikati ni msaidizi wa Balozi huyo, Liang Lin. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akimsikiliza Balozi mpya wa China nchini, Wang Ke, wakati balozi huyo alipokua anafafanua jambo katika mazungumzo yao yaliyofanyika katika ofisi ya Naibu Waziri huyo, jijini Dar es Salaam leo. Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walikubaliana kuendeleza ushirikiano zaidi kati ya China na Tanzania. Katikati ni msaidizi wa Balozi huyo, Liang Lin.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akimkaribisha ofisini kwake, Balozi mpya wa China nchini, Wang Ke (katikati), wakati balozi huyo alipomtembelea Masauni ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, kwa lengo la kujadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya China na Tanzania. Kushoto ni msaidizi wa Balozi huyo, Liang Lin.
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI,
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
No comments :
Post a Comment