AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, January 20, 2018

PICHA: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, Aondoka Nchini Zanzibar Kuelekea Nchini za Falme za Kiarabu (UEA)Kuaza Ziara Yake ya Kiserikali leo!

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika ukumbi wa VIP katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, kabla ya kuaza ziara yake ya Wiki Moja katika Nchi za Falme za Kiarabu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiagana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo 21-1-2018, akielekea katika Nchi za Falme za Kiarabu kuaza ziara yake ya Kiserikali ya Wiki Moja. 
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, wakati akiondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akiongozana na Mumewe Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,kushoto Makamu wa Rais wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiagana na Wazee wa CCM Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, akiondoka Zanzibar kuelekea katika ziara yake ya Wiki Moja katika Nchi za Falme za Kiarabu. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiagana na Viongozi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Zanzibar wakati akiondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, kuaza ziara yake ya Wiki Moja katika Nchi za Falme za Kiarabu.

/ZanziNews.

No comments :

Post a Comment