Magaidi wa Boko Haram nchini Nigeria, wamewauwa watu tisa katika mashambulizi mawili yaliyotekelezwa Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo. Boko Haram imeendelea kulaumiwa kote duniani na hatua zimeanza kuchukuliwa dhidi yake.Maafisa wa usalama wamethibitisha kutokea kwa mashambulizi hayo katika vijiji vya Jinene na Ngala katika jimbo la Borno.
Wapiganaji wa Boko Haram wamewauwa watu zaidi ya maelfu kwa kipindi cha miaka tisa sasa, na wengine zaidi ya milioni mbili kukimbia mkazi yao huku nchi hiyo ikiendelea kukumbwa na mashambulizi ya Boko HaramKundi hili limekua likijihusisha na mauaji na kuwateka nyara watu katika maeneo mbalimbali ambapo watu kadhaa wakiwemo wanafunzi wasichana wa chibok wanaendelea kushikiliwa na kundi hilo katika eneo lisilojulikana mpaka sasa.
No comments :
Post a Comment