Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, February 26, 2018

ZITTO KABWE AUMIZWA HUKUMU YA MBUNGE SUGU..ATOA MANENO MAZITO!

Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amefunguka na kuwataka Wabunge wa vyama vya upinzani wasimame mbele ili waweze kuhesabiwa ili wapate kujitambua wamebakia wangapi.

Zitto amebainisha hayo kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii baada ya kutolewa kwa hukumu ya Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA), Joseph Mbilinyi 'Sugu' na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga kwenda jela miezi mitano kutokana na kukutwa na hatia ya kutoa maneno ya fedheha dhidi ya Rais Magufuli.

"Nimeona mashtaka ya Sugu yaliyopelekea kuhukumiwa kwenda jela miezi 5. Wabunge wote wa vyama vya upinzani kwa namna moja ama nyingine tunasema haya kila wakati kwenye mikutano yetu. Kuna haja ya kufanya jambo ambalo dola itaamua kutusweka jela wote au kutorudia walichofanya kwa Sugu", amesema Zitto.

Kwa upande mwingine, Zitto amedai anawasiliana na wenzake ili waweze kupata 'united Democratic Front'.

No comments :

Post a Comment