dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, August 5, 2018

Baada ya mgombea wake kuenguliwa, CUF kufungua kesi Mahakamani!

Chama cha Wananchi CUF kimepinga na kulaani mpango wa kuenguliwa kwa mgombea wake wa udiwani kata ya Kimara, Abubakari Nyamguma isivyo kihalali katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Agosti 12 mwaka huu huku kikipanga kufungua kesi mahakamani kudai haki yao.
Wagombea watatu wa upinzani kutoka vyama vya upinzani Chadema, CUF na ACT Wazalendo waliondolewa kwa mapingamizi huku tume ya Uchaguzi NEC ikimtangaza kupita bila kupingwa mgombea wa CCM, Manota Pascal.

" Tunaamini kilichofanyika ni uonevu, hujuma na hatukutendewa haki katika utaratibu wa hoja zilizotumika kufikia maamuzi hayo ambayo kimsingi ni batili na ya kibabe kwani sababu iliyotolewa na mgombea wa CCM hazikuwa na ukweli na kushangaa msimamizi wa uchaguzi kuzikubali na kusema amejiridhisha kuwa mgombea wetu alikua na kosa la kiapo.

" Mgombea wetu alichukua fomu za udiwani fomu Na 8c kwa utaratibu ulioelekezwa na kanuni za uchaguzi na fomu hiyo ilijazwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na maelekezo ya uchaguzi ikiwemo kuapa mbele ya Hakimu wa mahakama ya mwanzo ya kimara na kufuata utaratibu wa mahakama wa kulipa malipo halali ya mahakama na kupewa stakabadhi ya Serikali Na. 16291712," alisema Mkurugenzi wa Uchaguzi wa CUF Wilaya ya Ubungo, Hamdani Kuangwa.

Hamdani amesema tayari wameshawasiliana na mawakili wao ili kuangalia namna ya kufungua kesi hiyo ili kuwawezesha wananchi wa Kimara kupata haki yao ya kumchagua mgombea wanaemtaka.

No comments :

Post a Comment