Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, August 15, 2018

Serikali yaidhinisha kuundwa kwa baraza la Kiswahili Kenya!


Baraza la Mawaziri nchini Kenya limeidhinisha kubuniwa kwa Baraza la Taifa la Kiswahili ambalo litatwikwa jukumu la kukuza na kuendeleza lugha hiyo nchini humo.

Pendekezo hilo linafuata kipengee 137 cha Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambacho kinasema kwamba lugha ya Kiswahili itaimarishwa, kukuzwa na kutumika kama lugha ya Jumuiya hii.

Baraza hilo litatumika kutoa ushauri, na vile vile kuimarisha maongozi ya serikali kuhusiana na kukuza, kulinda na kuunga mkono matumizi ya lugha ya Kiswahili na kushirikisha kazi ya mashirika ya kitaifa, kandaa hii, kitamaduni, mashirika ya elimu na mashirika mengine yanayohusika na lugha ya Kiswahili.

Wasomi wa Kiswahili na wadau wengine wamekuwa wakihimiza kuundwa kwa baraza hilo kwa muda mrefu.

Prof Hezron Mogambi ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi anasema hatua hiyo ni ya kupongezwa sana.

"Tumekuwa tukiingoja kwa muda mrefu kwa sababu maendeleo na makuzi ya Kiswahili yamekuwa yakikwazwa kwa sababu ya kukosa baraza kama hili. Matumizi sawa ya Kiswahili yamepigwa jeki," amesema.

Miongoni mwa mwengine, anasema baraza hilo litasaidia sana katika kuhakikisha kuwa hadhi ya Kiswahili kama lugha rasmi na ya taifa nchini Kenya na kwamba lugha hiyo "inazingatiwa na kuheshimiwa."

"Kwa sasa hakuna chombo cha kufanya hivyo. Kiswahili kimekuwa kikitumiwa nchini Kenya katika hafla na shughuli mbalimbali kwa njia isiyofaa. Hakuna wa kukosoa na kuelekeza. Matumizi sawa na upotoshaji utazuiwa kwa kuwa na chombo cha kufanya kazi hii," anasema.

No comments :

Post a Comment