Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, November 22, 2018

UCHOMAJI WA MAITI WAZUA WASIWASI WA MIZIMU ZIMBABWE!

Uchomaji wa maiti umeleta mjadala mkubwa nchini Zimbabwe, na kutaka mila na desturi pamoja na imani za kidini kuzingatiwa.

"Kwa kuwa tumeumbwa kwa mavumbi na mavumbini tutarejea'', mstari huu kutoka kwenye Biblia unaleta uzito kidogo kwa waumini wengi wa kikristo nchini Zimbabwe ambao wanapinga utaratibu wa kuchoma maiti.
Wanafikiri kwamba ni bora kuzika kawaida na wanahisi kwamba mwili utarejelea kwenye mavumbi kiasilia tu badala ya kuuharakisha kuurudisha mavumbini kwa kuuchoma.

Uchomaji wa maiti huwa unatumia joto linalokadiriwa kufika nyuzi joto 500 mpaka nyuzi joto 800.

Mjadala huo unaendelea kuchukua vichwa vya habari katika mji wa Bulawayo,ambao ni wapili kwa ukubwa nchini Zimbabwe na kwao ni lazima kwa maiti kuchomwa kwa wale ambao wanakufa wakiwa na miaka 25 kushuka chini.

Mapendekezo hayo yalikuja zaidi ya mwaka mmoja tangu halmashauri iliposema kwamba watoto wenye umri wa miaka 10 na walio chini ya hapo inabidi wachomwe ili kusaidia kuondoa changamoto inayowakabili watu wa mipango miji.

Ongezeko la watu katika maeneo ya miji nchini Zimbabwe unasababisha maeneo ya kuzika kukosekana.

 / BBC Swahili

No comments :

Post a Comment