Kwa maana hiyo Ikulu ya Marekani na umoja wa Ulaya wameshaipata hii. Asubuhi niliposoma Jamvi la habari nilitahadharisha kuwa hata hivi vijarida wanavisoma.
#Kosa kubwa ni kwamba EU na Marekani walitoa taarifa yao kupitia vyombo Rasmi na vya kisheria. Hapa kwetu kila MTU anajibu.
Mara Musiba ajibu, mpaka Sasa ma DC zaidi ya watano wameshajibu. Mawaziri wanapishana kujibu huyu Mchana yule Jioni.
Nachojiuliza ni je Serikali haina msemaji mmoja? Kwa nn tunaruhusu mambo Nyeti kama haya serikali kusemewa na watu ambao hawapo trained kwenye maswala ya Kidiplomasia?
Tutaendelea Kushauri..... Na ikiwezekana tuwapunguze wachumia tumbo waliokaribu na viongozi wetu ili wawekwe watu wanaofikiri kwa akili na sio matumbo.
Watu ambao watawasaidia viongozi wetu sio kujikomba. Kuna watu wamewakaribia kwa ukaribu mno viongozi wetu ambao hawana uwezo. Hawa Lazma idara yetu ya Usalama iwaweke mbali na Viongozi wetu.
Na wasiruhusiwe kujibu kwa niaba ya Serikali waiache Serikali ifanye kazi yake kupitia vyombo vunavyotambulika na kwa Kutumia wataalamu wake.
Ole Mushi
9712702602
https://zanzibarnikwetu.blogspot.com/2018/12/eu-parliament-calls-on-tanzania-to-end.html
https://zanzibarnikwetu.blogspot.com/2018/12/from-united-states-senates-committee-on.html
https://zanzibarnikwetu.blogspot.com/2018/12/baraza-la-seneti-marekani-serikali-ya.html
No comments :
Post a Comment