AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, January 28, 2019

Ujumbe wa Mfuko wa Khalifa Fund wa Abu Dhabi UAE Watembelea Kikundi cha Ushirika cha Faki Milling Enterproses Kisongoni Zanzibar.!


Mkurugenzi wa Ushirika wa Fakirice Milling Enteprises Kisongoni Wilaya Kaskazini B Unguja. Ndg Yussuf Faki Yussuf, akitowa maelezo ya Ushirika wao unaojishughulisha na usagaji wa mazao ya nafaka na mpunga, kwa Ujumbe wa Mfuko wa Khalifa Fund, uliotembelea Ushirika huo kuona maendeleo yake, wakiwa katika ziara yao Zanzibar. 

Ujumbe huo ukiongozwa na viongozi mbali mbali wa Serikali, ulifanya ziara ya kukitembelea kikundi cha ushirika cha ‘Tusizembee Cooperative’ kiliopo Kinaysini Kisongoni kinachojishughulisha na usagaji wa nafaka (mpunga).

Katibu wa Kikundi hicho Yussuf Faki Yussuf alisema ushirika huo hununuwa mpunga kutoka kwa wakulima na kuusaga na hatimae kuuza katika hoteli na maduka mbali mbali baada ya kufungwa vizuri katika mifuko maalum.

Alisema kwa wastani husambaza tani kumi (10) za mchele kila mwezi katika maduka hayo.

Alisema changamoto kubwa inayokabili ushirika huo ni ukosefu wa mtaji wa kuwezesha kununuwa kiwango kikubwa cha mpunga kutoka kwa wakulima.

Ujumbe huo uilipata fursa ya kuangalia jinsi mashine hizo za kusaga zinazofanyakazi pamoja na ubora wa mchele unaotolewa..

No comments :

Post a Comment