Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, March 14, 2019

Uingereza yazuiwa kuondoka EU bila makubaliano!

Wabunge wa Uingereza wamepiga kura kuizuia nchi hiyo kuondoka katika Umoja wa Ulaya bila ya kufikiwa makubaliano ya aina yoyote.

Wabunge 321 wamepiga kura kuipinga hatua hiyo huku 278 wakiunga mkono Uingereza kuondoka kwenye umoja huo kiholela, Kura ya jana imepigwa baada ya ile ya Jumanne, ambapo wabunge waliukataa mpango wa Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May kuhusu masharti ya nchi hiyo kuachana na Umoja wa Ulaya, maarufu kama Brexit.
Hatua ya Uingereza kuondoka bila ya makubaliano kuhusu uhusiano wa baadae kati ya pande hizo mbili, ingesababisha hatari kubwa katika biashara na mustakabali wa watu wa Uingereza na Umoja wa Ulaya.

No comments :

Post a Comment