dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, August 26, 2019

Waziri Mkuu wa Uingereza akutana na Rais Trump!

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson leo hii amefanya mazungumzo yake ya kwanza ya ana kwa ana na Rais Donald Trump wa Marekani tangu aanze kazi yake mpya.

Trump anamuunga mkono kiongozi huyo akimtazama kama mtu atakayeweza kufanikisha vyema hatua ya Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya, yaani Brexit.

Viongozi hao wamekutana kandoni mwa mkutano wa kilele wa kila mwaka wa viongozi wa nchi zinazoongoza kwa uchumi duniani, G7, unaofanyika mjini Biarritz, Ufaransa.
Alipoulizwa ana ushauri gani kwa Johnson kuhusu Brexit, Trump alijibu kwamba "Johnson hahitaji ushauri na ni mtu sahihi kwa kazi." Katika mkutano huo, Johnson pia alimtaka Trump kuviondoa vizuizi vya kibiashara kwa kampuni za Uingereza ili ziweze kuingiza bidhaa zao katika soko la Marekani, akisema vinahatarisha makubaliano ya biashara huria baada ya Brexit.

Rais huyo wa Marekani alijibu kwamba wanalifanyia kazi suala hilo na anafikiri litaweza kufanikiwa.

No comments :

Post a Comment