Watu chungunzima wamejeruhiwa na wengine wamenasa kwenye majengo kadhaa baada ya mripuko kuutikisa mji wa bandari wa Antwerp nchini Ubekgiji.
Taarifa hizo zimetolewa na polisi waliosema mripuko huo umeyaathiri majengo matatu katika wilaya ya Wilrijk eneo la kusini mwa katikati ya mji.
Kufikia sasa watu wawili wameokolewa kutoka kwenye kifusi kwa mujibu wa taarifa za zima moto zilizoandikwa kwenye ukurasa wa Twitta na kuongeza kwamba wanajitahidi kumuokoa mtu wa tatu.
Mbwa wa kunusa wanatumiwa kufuatilia watu waliotoweka katika mkasa huo.Hakuna taarifa za mara moja zilizotolewa na polisi kuhusu kilichosababisha mripuko huo uliotokea mchana,ingawa meya wa Antwerp Bart de Wever ameandika kupitia Twitta kwamba ni mripuko wa gesi.
Taarifa hizo zimetolewa na polisi waliosema mripuko huo umeyaathiri majengo matatu katika wilaya ya Wilrijk eneo la kusini mwa katikati ya mji.
Kufikia sasa watu wawili wameokolewa kutoka kwenye kifusi kwa mujibu wa taarifa za zima moto zilizoandikwa kwenye ukurasa wa Twitta na kuongeza kwamba wanajitahidi kumuokoa mtu wa tatu.
Mbwa wa kunusa wanatumiwa kufuatilia watu waliotoweka katika mkasa huo.Hakuna taarifa za mara moja zilizotolewa na polisi kuhusu kilichosababisha mripuko huo uliotokea mchana,ingawa meya wa Antwerp Bart de Wever ameandika kupitia Twitta kwamba ni mripuko wa gesi.

No comments :
Post a Comment