Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, October 10, 2019

Serikali ya Trump yakataa kutoa ushirikiano wa kumshitaki Rais!

Ikulu ya Marekani imesema serikali ya Rais Donald Trump haitatoa ushirikiano katika kile inachokiita uchunguzi usio halali wa kumshitaki rais uliopendekezwa na chama cha Democratic.

Katika barua iliyotumwa jana kwa viongozi wa bunge hilo mawakili wa serikali ya Trump wameeleza wazi kwamba hawatoshiriki.

Hatua ya kukataa kushiriki katika uchunguzi huo inaonesha kuwa Trump sasa anaweza kuingia katika mvutano wa kikatiba na bunge.
White House imesisitiza kwamba bunge halikupiga kura rasmi ya kuanza uchunguzi huo, na kuongeza kuwa kutokana na hilo linakosa mamlaka kamili ya kufanya mchakato wa kumshitaki Trump.

Akijibu barua hiyo spika wa bunge Nancy Pelosi amesisitiza kwamba bunge lina haki ya kikatiba ya kuzifuatilia taasisi za juu bila ya kuzingatia kura rasmi ya mchakato huo.

No comments :

Post a Comment