Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, October 13, 2019

Viboko wafaidika na ziara ya Rais Magufuli, Hatimaye wapelekewa maji!

Uongozi wa Hifadhi ya Taifa Mkoani Katavi (TANAPA) wamepeleka maji kwa ajili ya kuwasaidia viboko ambao  asili  yao hutegemea maji kama sehemu yao ya maisha

Ikiwa ni siku chache baada  ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano Dkt.John Pombe Magufuli kutoa agizo  kwa uongozi wa TANAPA mkoani humo kuhakikisha wanachimba bwawa na kuweka maji ili kuwasaidia wanyama hao aína ya viboko ambao asili ya maisha yao wanategemea maji kwa kiasi kikubwa.
"Ninawaagiza TANAPA muhakikishe mnachimba bwawa na mlijaze maji kuwasaidia hawa viboko wanateseka sana, unapokamua ng'ombe mpe na majani sasa nyie mnategemea kuingiza kipato kupitia hawa viboko halafu hamuwajali".

Pía Magufuli amewataka TANAPA kuanzisha bucha la nyama pori ambalo watauza aína mbalimbali ya  nyama ili kila mwananchi afaidike na kuwepo kwa Hifadhi mkoa kwake

Hata hivyo ametoa msamaha kwa vijiji 60 ambavyo vinapatikana ndani ya Hifadhi hio  kuendelea kuishi katika maeneo hayo na kuwataka kutohavunja sheria.

Takribani vijiji 920 nchi nzima vilivyo ndani ya Hifadhi ya taifa vimepewa kibari cha kuendelea kuishi katika maeneo yao bila kusumbuliwa.

Hifadhi ya Taifa mkoa wa katavi ni Hifadhi ya nne yenye eneo kubwa na nihifadhi ambayo Bado haijabadilika asili  yake licha ya kuwepo kwa migogoro baina  ya wakazi wanaoshi maeneo jirani na Hifadhi kuwazuru wanyama wanaotembelea kalibu na makazi ya watu

No comments :

Post a Comment