Watu sabini wamepoteza maisha katika mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa Kusini mwa Sudan.
John Abola, Gavana wa mkoa wa Boma kusini mashariki mwa nchi hiyo, amesema kuwa watu 70, wengi wao wakiwa ni watoto na wazee, wamekufa tangu mwezi Oktoba kutokana na mafuriko, na karibu nusu milioni ya raia wanahitaji msaada wa kibinadamu.
John Abola, Gavana wa mkoa wa Boma kusini mashariki mwa nchi hiyo, amesema kuwa watu 70, wengi wao wakiwa ni watoto na wazee, wamekufa tangu mwezi Oktoba kutokana na mafuriko, na karibu nusu milioni ya raia wanahitaji msaada wa kibinadamu.
Rais Salva Kiir Mayardit alitangaza dharura katika maeneo ya janga mwezi uliopita.
Nchini Sudani Kusini, ambako kumejaa maji kutokana na mvua kubwa tangu Oktoba, watu 800,000 wamepata shida ya njaa na magonjwa.
Nchini Sudani Kusini, ambako kumejaa maji kutokana na mvua kubwa tangu Oktoba, watu 800,000 wamepata shida ya njaa na magonjwa.
No comments :
Post a Comment