Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, July 23, 2022

USIKU MAALUMU WA AKINA MAMA WAWADIA JIJINI TORONTO!


Ule usiku uliokuwa ukingojewa na akina mama wengi wa ki-Zanzibari kutoka jijini Toronto na vitongoji vyake leo utawadia baada ya kuzama jua.

"Tupo tayari na maandalizi yote tushayamaliza", alielezea bi Shahida alipohojiwa na blog hili kuhusu usiku huu maalumu wa akina mama wa ki-Zanzibari wa Toronto.

"Nia ni akina mama kukutana pamoja na kubadilishana fikra na mawazo juu ya mambo mengi yanayoendelea duniani hivi sasa na katika maisha yetu", aliendelea bi Shahida Hamad ambae ndio kinara wa Management Team ya Zacadia ambayo imeudhamini usiku huu.

Zacadia ni moja katika Jumuiya za Wazanzibari wanaoishi nchini Canada ambayo makao makuu yake yapo mjini Toronto.


Bi Shahida alilijulisha blog hili kuwa..."ni wale tu waliokata tiketi kabla au waliopeleka mbele majina yao kuwa watakata tiketi mlangoni ndio wataruhusiwa kuingia kwenye hii party. Yoyote yule ambae hajatoa taarifa kuwa atakata tiketi yake mlangoni basi huyo hatoruhusiwa, kwasababu hii sio show bali ni special party na kwahivyo idadi ya wale watakaohudhuria ni lazima ijulikane mapema kwaajili ya matayarisho ya huduma za ndani", alimalizia bi Shahida.

Tokea Summer ya 2022 kuanza, Zacadia imekuwa mstari wa mbele katika juhudi za kuwakusanya Wazanzibari pamoja na shughuli yao itakayofuata baada ya hii ya leo kumalizika itakuwa ni picnic itakayofanyika tarehe 13 August kwenye ile Park inayopendwa sana na watoto katika jiji la Toronto iitwayo Earl Bales Park ambayo ipo kwenye barabara ya Bathurst nambari 4169.




No comments :

Post a Comment